Utangulizi
Unga wa mahindi ni chanzo kikubwa cha virutubisho kwa watu wengi Barani Afrika. Virutubisho kama vile wanga, protini, madini na vitamin hupatikana kutoka kwenye mahindi au unga wake.
Unga wa dona ni unga unaopatikana kwa kusaga mahindi bila ya kukoboa. Siku za hivi karibuni kumekua na uhimizo mkubwa sana wa matumizi ya unga wa dona na kufanya watu wengi kuanza kupunguza taratibu matumizi ya unga sembe au uliokobolewa.
Faida za unga wa dona

Udhibiti wa ubora katika hatua za utengenezaji wa unga wa dona
Dona yenye ubora na usalama inaweza kupatikana iwapo tu kunaudhibiti wa ubora katikatika mchakato wa utengenezaji. Udhibiti huo unatakia kuanzia mashambani, uvunaji, uhifadhi wa mahindi, hadi usagaji.
Nafaka zisipo vunwa, kukaushwa vizuri na kuhifadhiwa katika hali nzuri huweza kushambuliwa na wadudu waharibifu na vijidudu kama vile "fangasi" ambao mwisho wa siku huweza kusababisha nafaka au zao la nafaka kupungua ubora wake na kupata uambukizo wa "sumu kuvu" au kwa kitaalamu "aflatoxin". Aflatoxin huweza kuleta madhara makubwa kwenye miili ya binadamu kwa kusababisha cancer.
Vile vile iwapo udhibiti wa ubora hautazingatiwa katika hatua za uhifadhi hasa kwenye kuweka dawa za kuhifadhia mahindi "viatilifu" na usagaji wa mahindi. Kunauwezekano mkubwa sana kwa unga wa dona kubakiwa na kiwango kikubwa cha viatilifu au madawa ya kuhifadhia. Madawa hayo yanaweza kuwa ni sumu ambazo zinaweza zikamletea madhara makubwa mtumiaji wa unga huo. Kutokana na hilo basi ni muhimu nafaka zikahifadhiwa kwa mda unaofaa mara baada ya kuwekewa dawa kabla hazijafanyiwa mchakato mwingine wa kusagwa au kukobolewa.
Katika mashine za kusaga unga zilizopo kwenye maeneo yetu tunayoishi, suala la kuosha mahindi huwa halitiliwi maanani sana. Kutokana na ukweli kwamba mahindi mengi huwa yana kuwa na mabaki ya viatilifu suala la kuosha mahindi linatakiwa kuwa ni la lazima ili kuweza kuondoa au kupunguza kiwango cha madawa kilichopo kwenye mahindi.
Suala jingine la kujiuliza ni kwamba mara nyingi pumba za mahindi ndicho chakula kikubwa cha mifugo, lakini kiuhalisia sehemu ya nje ya nafaka/pumba za mahindi ndiyo sehemu ambayo huwa ina kiwango kikubwa zaidi cha dawa ili kuwazuia wadudu waharibifu. Kwahiyo mwisho wa siku sumu hizo huweza kuturudia kupitia mifugo.
Dona yenye ubora na usalama inaweza kupatikana iwapo tu kunaudhibiti wa ubora katikatika mchakato wa utengenezaji. Udhibiti huo unatakia kuanzia mashambani, uvunaji, uhifadhi wa mahindi, hadi usagaji.
Nafaka zisipo vunwa, kukaushwa vizuri na kuhifadhiwa katika hali nzuri huweza kushambuliwa na wadudu waharibifu na vijidudu kama vile "fangasi" ambao mwisho wa siku huweza kusababisha nafaka au zao la nafaka kupungua ubora wake na kupata uambukizo wa "sumu kuvu" au kwa kitaalamu "aflatoxin". Aflatoxin huweza kuleta madhara makubwa kwenye miili ya binadamu kwa kusababisha cancer.
Vile vile iwapo udhibiti wa ubora hautazingatiwa katika hatua za uhifadhi hasa kwenye kuweka dawa za kuhifadhia mahindi "viatilifu" na usagaji wa mahindi. Kunauwezekano mkubwa sana kwa unga wa dona kubakiwa na kiwango kikubwa cha viatilifu au madawa ya kuhifadhia. Madawa hayo yanaweza kuwa ni sumu ambazo zinaweza zikamletea madhara makubwa mtumiaji wa unga huo. Kutokana na hilo basi ni muhimu nafaka zikahifadhiwa kwa mda unaofaa mara baada ya kuwekewa dawa kabla hazijafanyiwa mchakato mwingine wa kusagwa au kukobolewa.
Katika mashine za kusaga unga zilizopo kwenye maeneo yetu tunayoishi, suala la kuosha mahindi huwa halitiliwi maanani sana. Kutokana na ukweli kwamba mahindi mengi huwa yana kuwa na mabaki ya viatilifu suala la kuosha mahindi linatakiwa kuwa ni la lazima ili kuweza kuondoa au kupunguza kiwango cha madawa kilichopo kwenye mahindi.
Suala jingine la kujiuliza ni kwamba mara nyingi pumba za mahindi ndicho chakula kikubwa cha mifugo, lakini kiuhalisia sehemu ya nje ya nafaka/pumba za mahindi ndiyo sehemu ambayo huwa ina kiwango kikubwa zaidi cha dawa ili kuwazuia wadudu waharibifu. Kwahiyo mwisho wa siku sumu hizo huweza kuturudia kupitia mifugo.
Nini cha kufanya?
1. Ili kuweza kuepukana na madhara haya ya sumu za kuhifadhia nafaka na sumu kuvu ni budi kwa watanzania kurudisha utamaduni wetu wa zamani wa kujiandalia vitu vyetu wenyewe. Andaa mahindi yako mwenyewe kwa kuyaosha na kuyakausha vizuri kabla ya kusaga badala ya kwenda dukani na kununua. Dona ambayo hujui imeandaliwaje kabla ya kusagwa inaweza ikakuletea madhara makubwa zaidi ya faida ulizodhani ungezipata. Baada ya kusaga unga hakikisha unaukasha vizuri kabla ya kuhifadhi.
1. Ili kuweza kuepukana na madhara haya ya sumu za kuhifadhia nafaka na sumu kuvu ni budi kwa watanzania kurudisha utamaduni wetu wa zamani wa kujiandalia vitu vyetu wenyewe. Andaa mahindi yako mwenyewe kwa kuyaosha na kuyakausha vizuri kabla ya kusaga badala ya kwenda dukani na kununua. Dona ambayo hujui imeandaliwaje kabla ya kusagwa inaweza ikakuletea madhara makubwa zaidi ya faida ulizodhani ungezipata. Baada ya kusaga unga hakikisha unaukasha vizuri kabla ya kuhifadhi.
2. Kupunguza matumizi ya pumba kwa mifugo, na kuanza kuipa vyakula muhimu au mbadala kama vile nyasi badala ya kuilisha pumba, kwani pumba hizo huwa zina masalia makubwa ya viatilifu.

No comments :
Post a Comment