Wednesday, July 1, 2015

MAKADA WA CCM ZAIDI WAPATAO 10 WAMESHARUDISHA FOMU ZAO

MAKADA maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamerejesha fomu na kufafanua mambo kadhaa ambayo yamekuwa yanazungumzwa juu yao kama njia ya kujiweka sawa kabla ya uteuzi kufanywa na vikao vikuu vya chama hicho. Waliorudisha fomu ni hawa wafuatao;
 
Mizengo Pinda
Mmoja wa waliorudisha fomu ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye wakati akirudisha fomu za kuomba kuteuliwa na kusema kuwa wanaochukulia suala la urais ni la kufa au kupona wana matatizo kwani anayejua Rais wa Tanzania ajaye ni Mungu.
Alisema safari yake ya kutafuta wadhamini ilikuwa na misukosuko mingi ikiwemo kutokea ajali tatu lakini hakuna ambaye alikuwa ameumia sana.
Akiwa ameongozana na mke wake, Tunu Pinda alisema mwana CCM mkomavu ni yule ambaye yuko tayari kukubali matokeo.
 
Alisema mpaka sasa ni wanachama wa CCM 42 waliojitokeza kugombea lakini katika hatua ya kwanza ni majina matano tu yatakayoteuliwa na kundi kubwa litaondolewa.
“Mimi sitegemei kwenye mchujo wa watu watano watokee watu wa kunung’unika kwani kila mtu aliyefika kuchukua fomu alikuwa anafahamu kuwa kutakuwa na mchujo kama tuko wengi wako watano kisha unakwenda ngazi ya pili, hakuna sababu ya kunung’unika,” alisema.
Alisema baadaye kuna kwenda kwenye Mkutano Mkuu atabaki mmoja. “Utanung’unikia nini? Kuna kushinda na kushindwa na kuna kupata na kukosa na ukisema suala la Urais ni kufa au kupona basi una matatizo, ifike mahali wana CCM wapate mtu ambaye wanadhani anaweza kusaidia kuongoza,” alisema.
Pia alisema waliojitokeza mwaka huu kuchukua fomu ni wengi. “Tuliojitokeza tusinuniane, kwa nini haniungi mimi mkono, na wewe usione jambo hili ni nongwa na usijione mapenzi ya Mungu yako kwako tu,” alisema.
Pia aliwataka viongozi wenzake washirikiane kumuunga mkono mgombea mmoja atakayepeperusha bendera ya CCM. “Anayejua rais wa Tanzania atakuwa nani ni Mungu peke yake,” alisema.
Mwakyembe arudisha fomu
Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe jana alirudisha fomu na kusema CCM itapata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu kutokana na kutekeleza ilani yake vizuri na wananchi kuwa na imani kubwa na chama hicho.
Mwakyembe ambaye alirudisha fomu jana mchana alisema katika safari yake ya kutafuta wadhamini mkoani ameweza kuwaona wanachama wengi wa CCM ambao wanaonesha imani kubwa na chama chao.
Alisema kila alipokutana na wana CCM waliojitokeza kumdhamini kwa tathmini aliyofanya tangu kuanza kwa siasa ya vyama vingi nchini CCM, itashinda ushindi wa kimbunga kwani mtaji upo kutokana na kazi kubwa iliyofanya serikali ya awamu ya nne katika utekelezaji wa ilani.
“Tumejipanga kuhakikisha wanaingia kwenye uchaguzi kifua mbele kutokana na kutekeleza ilani,” alisema. 
Pia alisema kwa upande wa pili wana kazi ya kuhakikisha yote mazuri yaliyofanywa na CCM yanasemwa.
 “Tuna kazi ya kuhakikisha kuwakumbusha wananchi barabara za lami na mafanikio mengi yamepatikana na serikali ya awamu ya nne ya CCM,” alisema.
Alisema kazi kubwa ni kuhakikisha umma unatambua CCM imefanya mambo mengi kutokana na upotoshaji unaofanywa na wapinzani kuwa CCM haijafanya lolote.
Pia alisema CCM kuwa na wagombea wengi waliojitokeza mwaka huu ni dalili njema za CCM kutoa fursa za kupatikana mmoja ambaye kila moja atamuunga mkono ili kuweza kukivusha chama.
Dk Mwakyembe alisema yuko tayari kumuunga mkono mgombea atakayeteuliwa na chama. Awali alisema amezunguka katika mikoa 15 katika kutafuta wadhamini.
Dk Mwele Malecela
Mwanachama mwingine wa CCM aliyerudisha fomu jana ni Dk Mwele Malecela ambaye alisema pamoja na kazi kubwa iliyofanywa katika uongozi wa awamu nne bado kuna watu wanaoishi kwenye umasikini uliokithiri.
Alitoa kauli hiyo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari. Alisema alifanikiwa kupata wadhamini katika mikoa 20 ikiwemo 17 ya Tanzania bara na mitatu ya Zanzibar.
Alisema wananchi wameonekana kufarijika kuona wanafuatwa kwenye maeneo ya kata walipo. Alisema ameweza kuzunguka mikoa tisa kwa siku nne hali inayoonesha kuwa kazi kubwa imefanyika katika ujenzi wa barabara za lami kuunganisha mikoa.
‘Pamoja na maendeleo na kazi kubwa ya awamu zote bado kuna umasikini uliokithiri lazima kuliangalia suala hilo kama kiongozi na kulitafutia ufumbuzi,” alisema.
Alisema aliguswa sana na wanawake waliojitokeza wakiwemo wazee ambao walikuwa wakitaka kumuona ni mwanamke wa aina gani ambaye anataka kugombea Urais.
“Wanawake wamefurahi sana kuona wanawake tunajitokeza hii ni fursa nzuri ya kuwapa moyo akinamama kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi,” alisema.
 
Membe Ayakana  Mabilioni  ya  Libya
Membe kwa upande wake wakati anarudisha fomu akijibu swali aliloulizwa kuhusu madai ya kuwa anahusika na ufisadi wa fedha za Libya na kama inavyosambazwa na wapinzani wake, alisema akigundulika kuwa alikula hata dola moja yuko tayari kujiuzulu.
“Uvumi kuwa nahusika na mabilioni ya Libya hauna mashiko kabisa baadhi ya wanasiasa wenzangu wanajua ukweli wote huu lakini kwa makusudi wameamua kuniunganisha na kampuni hiyo na kuwaaminisha watu ni yangu au nina hisa maneno hayo ni ya uongo,” alisema.
Alifafanua kuwa Libya ni moja kati ya nchi wafadhili wa Tanzania ambapo, kama ilivyo wafadhili wengine imekuwa ikiipa Tanzania misaada na mikopo yenye masharti nafuu.
Alisema katika utaratibu huo, Tanzania na Libya zilitia sahihi mkataba wa kubadili madeni na kuyaingiza katika miradi ambao uliweka utaratibu wa matumizi na urejeshaji wa fedha za deni la Libya.
Alisema kumbukumbu alizonazo zinabainisha kuwa kabla ya Serikali ya Libya kuweka saini katika mkataba wa nyongeza iliyotaka fedha hizo zikopeshwe kwa kampuni ya Meis, upembuzi yakinifu wa mradi husika ulifanywa kupitia vyombo vyake, na wao wenyewe kujiridhisha juu ya ubora wa mradi huo.
Sumaye na mahakama ya rushwa
 Naye Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ambaye naye alirejesha fomu alisema akichagulia kuwa Rais wa nchi ataanzisha mahakama maalumu ya wala rushwa.
Mbali na rushwa pia vipaumbele vyake ni pamoja na ufisadi, uhujumu uchumi na kwamba ataunda chombo cha uchunguzi katika masuala hayo.
Pia alisema wakati akiwa Waziri Mkuu wa Tanzania alifanya mambo makubwa na atahakikisha anaunda serikali inayofahamu kutimiza wajibu wake.
‘Uchumi ninaouzungumzia si wa takwimu ni wa hali halisi, nitaangalia pia maeneo kama viwanda vikubwa na vidogo ili watu wengi waweze kujiajiri na kulinda viwanda vya ndani,” alisema.
Alisema atahakikisha uzalishaji wa viwanda vya ndani unaongezeka na kunakuwa na ongezeko la mauzo ya nje ya nchi. Pia alisema ataimarisha huduma za jamii, ikiwemo elimu, afya upatikanaji wa maji na huduma nyingine muhimu.
Alipohojiwa kama maeneo aliyokwenda kutafuta wadhamini aliombwa rushwa, Sumaye alisema, tangu aanze kazi ya siasa hajawahi kutoa rushwa.
“Hata maeneo ambayo nimekwenda kutafuta wadhamini sijatoa fedha hata zilizodaiwa kwa lugha laini nilikataa kwani nilitaka nidhaminiwe na wale walio na imani na mimi,” alisema.
Alisema wakati akiwa Waziri Mkuu alipambana na wala rushwa ambapo aliweza kuwafukuza kazi watu 3,360 huku wengine 400 walipelekwa mahakamani.
Balozi Mahiga
Balozi Mahiga naye wakati anarejesha fomu alisema ameenda mikoa 15 kwa gari na akawashukuru wana CCM kumlaki na kwamba wamehamasika na wanasubiri kwa hamu uchaguzi.
 
Alisema kama CCM ikimpitisha kuwa mgombea atahakikisha kuwa anajenga maadili ya uongozi ili kuondokana na vitendo vya rushwa na ufisadi.
 
Alisema uongozi mzuri ni ule unaojengwa katika misingi ya maadili na atapambana na rushwa ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikirudisha nyuma wananchi.
“Nitahakikisha ninaimarisha misingi ya umoja na mshikamano katika nchi ikiwa ni pamoja na kudumisha muungano wa Tanzania na Zanzibar,” alisema.
Joseph Chaggama
Mwanachama mwingine wa CCM aliyerudisha fomu jana ni Joseph Chaggama ambaye alisema amezunguka katika mikoa 17 wakati wa kutafuta wadhamini. Alisema anaijua CCM vizuri na jinsi Serikali inavyoendeshwa.
 
Aliongeza na kusema yeye ni mmoja wa watu wasiofahamika na sababu ya kuchukua fomu ni nia ya dhati kutoka moyoni kuwa anaweza kuongoza nchi.
Pia alisema uwezekano wa yeye kuchaguliwa lazima kutokee muujiza. Alisema yuko tayari kuwatumikia Watanzania ikiwa atapewa ridhaa ya kuwa mgombea wa CCM na akashinda uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu na kuwa yuko tayari kumuunga mkono mgombea ambaye atateuliwa na chama.
 
Monica Mbega
Mbunge wa zamani wa Iringa Mjini, Monica Mbega naye alirudisha fomu na kusema kuwa chama kiliweka utaratibu mzuri wakati wakienda mkoani kupata wadhamini katika mikoa 15 ikiwemo mitatu ya Zanzibar.
Alisema amekamilisha kazi yake kwa ukamilifu bila matatizo na kuwashukuru wanawake wengi waliojitokeza kumuunga mkono.  Aliongezea pia na kusema suala la rushwa linategemea jinsi mtu alivyokwenda wakati akitafuta wadhamini
 
Amos akemea matumizi makubwa ya fedha
Mwingine aliyerudisha fomu hizo jana ni Amosi Siyantemi ambaye ni mtumishi wa CCM wakati ambaye alisema kuwa kwenye mchakato wa kutafuta wadhamini baadhi ya wagombea wameonesha matumizi makubwa ya fedha.
“Ni jambo la kujiuliza fedha hizo wamepata wapi na ni kiasi gani ni lazima wachunguzwe na kuchukuliwa hatua,” alisema Siyantemi.
Pia alisema rushwa ni ugonjwa mbaya unaoiangamiza jamii ni lazima zichukuliwe hatua za haraka na makusudi ili kuweza kukomesha suala hilo kabla nchi haijatumbukia kwenye shimo la machafuko.
Alisema CCM ya sasa si kama ile ya Mwalimu Nyerere. “Tunahitaji kurejesha haraka heshima ya CCM machoni mwa Watanzania na kwenye macho ya Jumuiya ya Kimataifa,” alisema.
Alisema akichaguliwa kuwa Rais atahakikisha kunakuwa na huduma bora za matibabu sanjari na bima ya afya kwa kila Mtanzania, kufanya mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa elimu kwa kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kupunguza idadi ya masomo.
 
Pia alisema atapiga marufuku mauzo na manunuzi yanayofanyika nchini kwa malipo ya dola ambapo malipo ya dola yatafanyika kwa kibali maalumu.
 
Pia alisema atakuwa na jukumu la kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya sanaa, michezo na burudani yatakayolenga kuwanufaisha kiuchumi wananchi.

Tuesday, June 30, 2015

Wabunge 33 wapitisha muswada bungeni

Dodoma. Wabunge 33 jana walipitisha Muswada wa Benki ya Posta Tanzania (kufuta sheria iliyoanzisha Sheria ya Benki ya Posta na kuweka masharti ya mpito).
Idadi ya wabunge wote ni 356 na nusu yake ni 178 wanaotakiwa kupitisha jambo lolote lenye uamuzi ikiwamo miswada.
Tangu asubuhi jana, kulionekana kuwa na idadi ndogo ya wabunge huku baadhi yao wakiingia na kutoka kila walipomaliza kusaini mahudhurio.
Mara baada ya kupitishwa kwa muswada huo ambao uliwasilishwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, idadi ya wabunge ilipungua zaidi na kubaki wabunge 29 huku Muswada mwingine wa Sheria ya Masoko ya Bidhaa wa 2015 ulipokuwa ukiwasilishwa na Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima.
Wakati hali ikiwa hivyo ndani ya Ukumbi wa Bunge, kulikuwa na idadi ndogo ya wabunge walioonekana nje ya ukumbi wakizungumza kwa vikundi na wengine wakiwa ‘bize’ na simu zao za mikononi.
Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Habib Mnyaa alilalamikia kitendo hicho akisema ni uvunjaji wa kanuni na Katiba ya nchi.
Mnyaa alisema kuwa wabunge wa Tanzania wengi ni wapole na wasiopenda makuu kwani kama ingetokea mtu yeyote akasimama na kuamua kushtaki, lazima angeshinda na kupata umaarufu mkubwa.
“Hapa tunachokifanya siyo jambo jema hata kidogo, unajua mambo mengi tunayopitisha hapa yanakuwa sheria. Si sahihi na tunaanza kuvunja sheria sisi wenyewe humu ndani,” alisema Mnyaa.
Alisoma Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 94 (1) ambayo inaeleza kuwa upitishwaji wa jambo lolote linalohusu uamuzi wa wabunge ni lazima akidi iwe ni nusu ya wabunge wote kama ilivyo Kanuni ya 77 ya Bunge.
“Kila tukisema sisi tunapingwa na kuambiwa kaa chini, tena sisi wapinzani ndiyo shida kweli na hasa hawa wanaokalia viti (anawataja) wanatubana sana ni afadhali na Ndugai (Job, Naibu Spika),” alisema.
Mbunge huyo alibainisha kuwa wakati wowote kama ataibuka mtu wa kutaka kuliburuza Bunge mahakamani, atashinda kesi hiyo mchana kweupe na sheria nyingi zitapaswa kufutwa.

Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano, 2015/ 2016


OWM-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015. Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali.

Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi.

 
Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 nawavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansina Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 nawavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomoya Sanaa na Biashara.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2015 wataanza muhula wa kwanza tarehe 18 Julai, 2015 na hakutakuwa nafursa ya mabadiliko yoyote ya shule. 

 
Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya mwisho yakuripoti, nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine aliyekosa nafasi.

Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi mwaka 2015 inapatikana kwenye tovuti ya OWMTAMISEMI
ya www.pmoralg.go.tz, au
Bofya HAPA
 

Monday, June 29, 2015

Watangaza nia ya Uraisi CCM wafika 42

Tokeo la picha la WATANGAZA NIA CCMMWANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Banda Sonoko, jana amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama hicho ili kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu ujao akiwa ni mgombea wa 42.
Baada ya kuchukua fomu hiyo jana, Sonoko alisema kama chama hicho kitampitisha kuwa mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu ujao na kushinda, moja ya vipaumbele vyake ni pamoja na kuzingatia misingi imara ya ilani ya 2005 pamoja na kuondoa umaskini kwa Watanzania.

Sonoko amewahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwemo ya Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Temeke ambapo katika kampeni zake za kusaka urais atatumia kauli mbiu inayosema "Kutokomeza Umaskini".

Alisema akiingia Ikulu, atawatimizia Watanzania mahitaji mbalimbali ambayo wameyakosa muda mrefu ambapo yeye ana sifa zote za kuwa rais ndio maana ameamua kuchukua fomu.

Aliongeza kuwa atahakikisha nchi inaendeshwa kwa kodi za wananchi si misaada kutoka nchi wahisani ambapo wanawake watawezeshwa katika mambo mbalimbali na kupewa nyadhifa kwenye vyombo vya maamuzi pamoja na vijana.

Sonoko alisema Serikali ambayo ataiongoza itasimamia haki, kupinga vitendo vya utoaji na upokeaji rushwa hasa Mahakamani ambapo kesi zitakuwa zikiendeshwa kwa muda maalumu, kurudisha viwanda, kuinua kilimo na kuboresha miundombinu.

"Nitahakikisha kila Wilaya inakuwa na sehemu yake ya kuegesha magari, kuongeza ajira na kuwasaidia vijana," alisema na kuongeza kuwa, hadi Julai mosi, mwaka huu, atakuwa amekamilisha taratibu za kupata wadhamini 450 katika mikoa 15.

NAFASI YA KAZI: Special Needs Teacher : Haven of Peace Academy (HOPAC)


The mission of Haven of Peace Academy (HOPAC) is to provide an excellent, Christ-centred, international education that meets western academic standards and equips students to live out a biblical worldview in all areas of life to the glory of God.
Haven of Peace Academy is seeking a Special Needs Teacher for the 2015/2016 school year. School year: August – June with classes Monday to Friday. HOPAC follows the Cambridge curriculum.
HOPAC, founded in 1994, is an international Christian K-12 school with over 300 students from 33 different countries and a variety of religious backgrounds including Christian, Muslim and Hindu. While the majority of students come from families of missionaries and the non-profit and international business community, one third are Tanzanian.
HOPAC teachers must be committed Christian, 55 years of age or younger with Bachelor degree, at least 3 years of teaching experience and fluency in English. HOPAC expects teaching staff to be supported spiritually and financially through a mission organization or home church. The school provides volunteer staff assistance in the form of a monthly living allowance that covers a significant portion of monthly in-country expenses.
Qualifications:
- Bachelors Degree
- Evangelical Christian
- 3+ years experience

How to apply

Please email Cover Letter and CV to personnel@hopac.net
Kindly state the job posting in the email subject line

Lipumba asema CCM hakiwezi kutoa rais mwadilifu

Mara. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amesema CCM hakina kiongozi mwadilifu atakayeweza kupeperusha bendera ya nchi, kutokana na viongozi wake kugubikwa na ufisadi.
Profesa Lipumba alitoa kauli hiyo jana kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo mjini Musoma alipokuwa akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara.
Alisema lengo la mkutano huo ni kuwaelimisha wananchi kuchagua viongozi wenye uadilifu na wanaojali rasilimali za nchi na watu wake badala ya kuchagua viongozi ambao ni mafisadi na wasio na uchungu wa kuinua pato la Tanzania.
Alisema anaunga mkono kauli ya mtoto wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Makongoro kuwa CCM kimekamatwa na kimekumbatiwa na vibaka ambao hawataki kuondoka ndani ya chama kwani wamekwishaweka mizizi.
“Nyerere atambue kuwa vibaka wakishang’ang’ania hawatoki na hata hayati Baba wa Taifa angekuwa hai angekuwa upinzani, hakika nawaeleza,” alisema Profesa Lipumba.
Alisema anawashangaa viongozi wa CCM ambao wanataka kuongoza nchi wakati walishindwa kuwatetea Watanzania katika Bunge la Katiba ili ipatikane Katiba bora.
“Hawa waliweka masilahi mbele na kulinda nafasi na madaraka ya viongozi, kumbe lengo lao ni kuendelea kuwanyonya wananchi,” alisema.
“Katiba ile ilikuwa inampunguzia madaraka rais na pia ilikuwa inawapa wabunge nguvu ya kuihoji Serikali, ilipinga waziri kuwa wabunge ili Bunge liwe huru kujadili Serikali,” alisema.
Pia alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kujiandikisha kwa wingi na kuhakikisha kipindi cha kupiga kura kitakapofika, wachague wagombea wa Ukawa ili wanaodai kuwa haipo wapate kuijua.
Alisema kama isingekuwa sheria, vyama vyote vya upinzani vingekuwa chama kimoja na kupeperusha bendera ya Ukawa katika kuchagua viongozi kuanzia ngazi za udiwani, ubunge na urais.
“Nimetangaza nia nitagombea urais, lakini nasubiri kwanza Ukawa iamue ni nani anayefaa kugombea kupitia umoja huu, hata kama si mimi, nitahakikisha atakayepitishwa nitampigia kampeni ili nchi isiende kwa mafisadi,” alisema.