Saturday, June 27, 2015

Majambazi waua Askari...Wapora fedha Benki ya NMB

Tokeo la picha la ak 47
Watu kadhaa wanao daiwa kuwa ni majambazi jana  walivamia Benki ya NMB tawi la Mkuranga mkoani Pwani na kupora fedha kisha kumuua askari mmoja na kutokmea kusikojulikana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jafary Mohamed alithibitisha jana  jioni  kupata taarifa za tukio hilo.
 “Taarifa hizo nimezipata kuwa watu hao wanaodhaniwa majambazi wamevamia  Benki ya NMB, Mkuranga na kupora fedha ambazo kiasi chake bado hakijafahamika kisha kumuua askari mmoja aliyekuwa nje ya uzio wa eneo hilo la benki," alisema Jafary  .
Hata hivyo alisema askari aliyeuawa   hakuwa kazini ila walinzi wote wa benki wapo salama na silaha zao hazikuchukuliwa.
 

No comments :

Post a Comment