Sunday, July 5, 2015

Zitto Kabwe Awataja Walioficha Mabilioni ya Fedha Uswisi

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo katika viwanja  vya Mwembeyanga jana amewataja watanzania walioficha mabilioni ya Fedha  katika Benki za nje ya nchi.
 
Akizungumza na  wakazi wa jiji la Dar es salaam Zitto Kabwe amesema  hivi sasa  uchumi wa nchi umeshikwa na watu wachache hususani wafanyabiashara ambao pia wameshika siasa au kwa wao kushiriki kwenye siasa moja kwa moja au kufadhili wanasiasa wa kutetea maslahi yao.
Ameongeza kuwa nchi ina Kansa ya Ufisadi ambapo  watu hutumia nafasi zao za uongozi kujilimbikizia mali ikiwemo  viongozi walioshika madaraka ya umma.
Mwezi Novemba mwaka 2012 Bunge lilipitisha Azimio namba Tisa la Mwaka 2012 ambalo lilielekeza Serikali kufanya uchunguzi kuhusu Watanzania na makampuni ya kitanzania waliotorosha na kuficha fedha kwenye mabenki ughaibuni
Uchunguzi pia ulikuwa uhusike na Mali za Watanzania zilizopo nje ya nchi katika juhudi za kuhakikisha kuwa fedha chafu na ufichwaji wake vinakomeshwa. Bunge lilitoa muda wa miezi sita kwa Serikali kufanya uchunguzi huo.
 
Mwaka mzima ulipita Serikali haikutoa maelezo yeyote na baada ya kubanwa ndani ya Bunge Serikali ikaomba miezi sita zaidi. Hata hivyo mpaka leo Serikali haijatoa kauli yeyote kuhusu taarifa hiyo ya uchunguzi.
 
Ametolea mfano kuwa  taarifa ya Serikali ya kisiwa cha Jersey kilicho chini ya himaya ya Uingereza inaonyesha kuwa Fedha na Mali za Watanzania katika mabenki kisiwani humo ni paundi za Uingereza 440 milioni ambazo kwa bei ya sasa ni sawa na shilingi za kitanzania 1.4 trilioni.
 
Vile vile taarifa rasmi ya Benki Kuu ya Uswiss inaonesha kuwa Watanzania wenye akaunti katika mabenki ya nchi hizo imefikia dola za kimarekani 304 milioni kutoka dola 213 milioni mwaka 2012. Amesema  hana takwimu kwa nchi nyingine duniani huku akisistiza kuwa fedha hizi  zilizofichwa zaweza kuwa halali au haramu.
 
Amesisitiza kuwa Serikali imenyima haki hiyo kwa zaidi ya miaka miwili na nusu sasa. Bunge la Kumi linavunjwa mnamo tarehe 9 Julai mwaka huu na hakuna dalili yeyote ya Serikali kutoa taarifa ya uchunguzi ndani ya bunge kama ilivyoagizwa na Bunge.
 
Orodha hiyo amesema ali iwaslisha  kwa Gavana wa Benki Kuu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa ajili ya uchunguzi lakini Serikali mpaka sasa  haijatoa taarifa licha ya kupewa kila aina ya ushirikiano.
 
“Nimeamua leo kuiweka orodha hii wazi kama shinikizo kwa Serikali kutoa taarifa ya uchunguzi kabla ya Bunge kuvunjwa wiki ijayo.”Amesema Zitto
 
Orodha hiyo ina majina 99 ya Watanzania au watu wenye mahusiano na Tanzania ambao wana akaunti HSBC ya Uswiss. Jumla ya akiba katika akaunti Benki hii pekee ni dola za kimarekani 114 milioni. 
 
Orodha hiyo ipo kama inavyoonekaa hapo chini:
 
 
 
 

Warioba: CCM ina kazi ngumu kumpata mgombea urais

 
Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba; picha kutoka maktaba

Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba amesema CCM inakabiliwa na kazi ngumu ya kupata mgombea wa urais atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi wa mwaka huu, akionya kuwa makundi ya urais yasipomalizwa yanaweza kufika hadi ngazi ya kata.
Makada 38 wamejitokeza kuomba ridhaa ya chama hicho tawala ya kugombea urais katika kipindi ambacho kuna ongezeko kubwa la nguvu ya vyama vya upinzani, huku vyama vinne vikiwa vimeamua kusimamisha mgombea mmoja.
Tayari vikao vya kujadili jinsi ya kumpata mteule wa kupeperusha bendera ya chama hicho vimeshaanza kwa wenyekiti na makamu wao kukutana na jana Kamati Kuu ilikuwa inakutana mjini Dodoma.
Akiangalia hali hiyo, Jaji Warioba aliiambia Mwananchi jana kuwa chama hicho tawala kinatakiwa kuwa makini katika mchakato huo, kwa maelezo kuwa unaweza kuacha majeraha makubwa kutokana na makundi yaliyoibuka.
“CCM inakabiliwa na wakati mgumu wa kupitisha jina la mgombea urais kutokana na waliojitokeza kuwania nafasi hiyo kufikia 38, na mpaka sasa imekuwa ni vigumu kutabiri atakayepitishwa, jambo ambalo halikujitokeza wakati wa upitishwaji wa mgombea urais wa chama hicho mwaka 1995 na 2005,” alisema Jaji Warioba, ambaye alikuwa mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Alisema kila unapofika Uchaguzi Mkuu kunakuwa na changamoto zake, lakini mwaka huu CCM inakabiliwa na changamoto kubwa zaidi kwa sababu uchaguzi huo utamleta rais mpya na mwenyekiti mpya wa chama hicho.
Alisema jambo la kwanza lililotokea katika mchakato wa kumpata mgombea urais litakalokifanya chama hicho kuwa na wakati mgumu ni kitendo cha baadhi ya wagombea kueleza sera zao, wakati wakijua wazi kuwa sera za CCM ziko kwenye ilani yake ya uchaguzi.
“Waliotangaza nia wamekuwa wakieleza sera zao na ukiwasikiliza unaona kama walikuwa wagombea binafsi hivi kwa sababu CCM ina sera, wanayo ilani ambayo ipo tayari na yeyote atakayepeperusha bendera ya CCM lazima ajikite kwenye ilani ya chama,” alisema jaji Warioba.
“Kama mtu ametangaza sera na vipaumbele vyake na havifanani na vipaumbele vya ilani ya chama unafanyaje? Ni mtihani mwingine huo.”
Alisema jambo la pili ni kukiukwa kwa utaratibu uliowekwa na chama hicho kwamba yeyote anayehusika kwenye ngazi ya maamuzi, asimdhamini mgombea yeyote wa urais, huku akiwatolea mfano wajumbe wote wa mkutano mkuu wa chama hicho ambao ndio humchagua mgombea urais wa chama hicho.
“Nimeambiwa kwamba wajumbe wa mkutano mkuu walikatazwa kudhamini wagombea, lakini tulivyoona ni kwamba viongozi wengi wameonyesha waziwazi wapo kundi gani, wapo waliojitokeza na kusema na wengine hawakusema lakini wanajulikana wanamuunga mkono mgombea gani,” alisema.
“Hawa ndio watakwenda kuchuja, sasa hapa itakuwa kazi ngumu na inawezekana kukawa na mgongano wa maslahi na hilo lisipoangaliwa linaweza kufanya mchujo ukaonekana kuwa haukuwa wa haki. Jambo hili linatakiwa kuangaliwa na hasa kwa kuwa kuna makundi.
 
Alisema makundi yaliyoibuka ndani ya chama hicho yanaweza kuifanya CCM ikalegalega na hasa kama wengine watafikiri utaratibu uliotumika wa kumpata mgombea haukuwa wa haki.
“Hali hiyo ikitokea itakuwa ngumu kuyarudisha makundi hayo ili kuwa kitu kimoja,” alionya Jaji Warioba ambaye pia aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
“Katika siasa chama ndiyo muhimu na kisipokuwa imara, mgombea yeyote wa chama husika hataweza kuwa na nguvu sana. Nadhani itasababisha matatizo na si katika urais tu, haya makundi yasipopatana yakaendelea na uhasama itakwenda mpaka kwenye majimbo na kata,” alisema.
Alisema mwaka huu ni wa ushindani na kama CCM isipochukua tahadhari katika kumpata mgombea, chama hicho kitakumbana na wakati mgumu.
Kamati Kuu ya CCM itakutana Julai 9 kufanya mchujo na Julai 10 Halmashauri Kuu itakutana kupanga ajenda za Mkutano Mkuu ambao utafanyika Julai 11-12 kwa ajili ya kumchagua mgombea urais.
Kamati Kuu, ambayo ndiyo msingi wa maamuzi yote, inaundwa na mwenyekiti, ambaye ni Rais Jakaya Kikwete; mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein; Makamu mwenyekiti, Philip Mangula; katibu mkuu, Abdulrahman Kinana; makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal; Waziri Mkuu, Mizengo Pinda; Spika Anne Makinda na Balozi Seif Ali Iddi.
Wengine ni Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Amir Kificho; Rajab Luhwavi, Vuai Ali Vuai, Nape Nnauye, Mohamed Seif Khatibu, Zakhia Meghji, Asha Rose- Migiro, Sophia Simba, Sadifa Juma Khamis, Abdallah Bulembo, Jenister Mhagama, William Lukuvi.
Wengine ni Steven Wasira, Dk Emmanuel Nchimbi, Pindi Chana, Jerry Silaa, Adam Kimbisa, Shamsi Vuai Nahodha, Dk Hussein Mwinyi, Maua Daftari, Samia Suluhu, Dk Salim Ahmed Salim, Makame Mbarawa na Hadija Abood.
Msekwa anena
Wakati Jaji Warioba akitafakari mustakabali wa CCM, makamu mwenyekiti wa zamani wa chama hicho, Pius Msekwa amesema ukiukwaji wa kanuni na taratibu za uchaguzi itakuwa ni moja ya mambo mawili makubwa yatakayoangaliwa kwenye mchujo wa wagombea.
Mbali na ukiukwaji huo wa taratibu, watatumia vigezo 13 vilivyowekwa na chama hicho kumpata Rais wa Serikali ya Awamu ya tano na mwenyekiti wa chama hicho.
Tayari baraza hilo linaloongozwa na Rais wa Serikali ya Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi limeripotiwa kuanza kazi ya uchambuzi na litawasilisha taarifa yake kwa Kamati Kuu .
 
Wajumbe wengine wa baraza hilo la wazee ni Rais wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, marais wa zamani wa Zanzibar Aman Abeid Karume na Dk Salmin Amour.
Jana, Msekwa ambaye amewahi kuwa makamu mwenyekiti wa CCM-Bara, alisema kazi hiyo itafanywa kwa umakini mkubwa kwa kuzingatia mambo hayo mawili.
“Sifa zimeandikwa kwenye kanuni zetu za chama na zipo 13. Hizo ndizo zitakuwa kipimo cha wagombea katika vikao na watachujwa kwa kuzingatia hilo. Ni lazima kutazama kama mgombea ana sifa hizo,” alisema.
“Pili, tunatazama kama mgombea amekiuka masharti yoyote ya kanuni zetu maana unaweza kuwa na sifa lakini ukawa umekiuka masharti.”
Alisema mambo hayo mawili ndiyo yatakayotumika na hakuna kigezo kingine chochote kitakachomfanya mtu kupata au kukosa nafasi.
Msekwa alikumbushia makada wa chama hicho waliowahi kukumbana na adhabu baada ya kukiuka masharti ya kanuni akisema: “Nadhani unakumbuka wapo waliowahi kusimamishwa kutokana na kukiuka masharti ya kanuni baada ya kuanza kampeni mapema. Kwa sasa wameshafunguliwa.”
Makada waliopewa ‘adhabu ya kifungo’ cha mwaka mmoja kutokana na kujihusisha na kampeni za urais kabla ya wakati ni mawaziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Waziri wa Kilimo na Ushirika, Steven Wasira.
Wengine ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
 
Source: Mwananchi

UPDATES: Risasi zarindima BVR, mkutano ZEC wavunjika

Mmoja wa majeruhi waliyopigwa risasi ,Ramadhani Hija Hassan akiwa katika kituo cha afya cha AL-Rahma kwa ajili ya kupatiwa matibabu .Alipigwa risasi wakati wa vurugu zilizotokea kwenye kituo cha kuandikisha wapiga kura cha Shehia ya Nganani Mjini Magharibi, Unguja jana.Picha na Talbu Ussi.
Zanzibar. Wakati watu watano wakijeruhiwa, wawili kwa kupigwa risasi, kwenye uandikishaji wa wapigakura eneo la Makunduchi, mkutano baina ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar na wadau umevunjika kutokana na mzozo wa mgwanyo wa majimbo.
Vurugu hizo zimetokea baada ya watu waliokuwa wamekusanyika katika Msikiti wa Kubini kwa madhumuni ya kupinga kazi hiyo ya uboreshaji wa Daftari la Wapigakura wakituhumu kuwapo kwa mamluki waliokuwa wakiandikishwa, lakini wakajikuta wakivamiwa na kundi la askari wasiokuwa na sare ambao walikuwa na silaha za moto.
Waliojeruhiwa kwa risasi ni Kheri Makame Hassan (42) na Ramadhani Hija Hassan (29) wote wakazi wa Makunduchi wakati Ali Seif Issa (38), Ali Hassa Hassan (70) kutoka Paje akiwa amepigwa kwa magongo na nondo na kuumia vibaya miguuni, na Hassan Ali Ameir (43).
Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti hospitalini hapo, majeruhi wao walisema walikuwa katika kituo cha Nganani, Shehia ya Nganani Kusini Unguja ndipo walipokuja watu waliovaa vinyago na kuwaamuru waondoke eneo hilo wakati uandikishaji ukiendelea.
“Ilikuja gari na watu waliojifunika nyuso zao wakatuambia tuondoke na sisi tukakataa kwa sababu tulikuwa tunazuia kuandikishwa mamluki katika eneo letu. Baada ya kubishana pale wakaenda kuchukua gari nyingine wakaanza kutupiga,” alisema Kheri ambaye amepigwa risasi ya pajani.
“Watu waliojifunika nyuso walikuja mara mbili na kuondoka kabla ya kufanya shambulio na kufanikiwa kuondoka katika eneo la tukio la Nganani kwa kutumia magari mawili,’ alisema Faki huku akilalamika kusikia maumivu.
Shuhuda wa tukio hilo, Ameir Mussa, mkazi wa Makunduchi, alisema kwamba waliamua kukusanyika eneo la msikiti wakitafakari jinsi ya kuzuia uandikishaji wa wapigakura mamluki, ambao ni pamoja na walio na umri mdogo.
“Lilikuja kundi la watu mara mbili na kuondoka. Walikiwa wamefunika nyuso zao na waliporudi kwa mara ya mwisho walitushambulia kwa kutumia silaha za kienyeji na baadaye kufyatua risasi za moto na kujeruhi watu wawili,” alisema Mzee Ameir.
Daktari wa zamu wa Hospitali ya Al Rahma, Seif Suleiman alithibitisha kupokea majeruhi na kusema kwamba katika hatua za awali wanazuia damu kuvuja kutoka kwenye majeraha.
Alisema wanaendelea na vipimo ili kujua majeraha hayo yamesababishwa na nini. “Tumewafanyia x-ray ili kujua majeraha yao yanatokana na nini lakini yanaonesha wazi kuwa ni majeraha kama ya risasi kwa kuwa risasi jeraha lake linakuwa ni kitobo kidogo inapoingia lakini kitobo kikubwa inapotokea risasi.” Dk Suleiman alisema majeruhi hao wanaendelea vizuri baada ya kutibiwa na wengine wataruhusiwa watakapopata nafuu.
“Wapo walioumia sana hao wataendelea kuwepo hospitali kwa sababu wametokwa damu nyingi sana na kutoka Makunduchi hadi Mjini ni mbali kwa hivyo wanahitaji kupumzishwa kwanza hadi hapo watakapopata nafuu,” aliongeza Dk Suleiman.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kusini Unguja, Juma Saadi alisema kuwa katika mkoa wake kuna uandikishaji wananchi kuwaingiza kwenye Daftari la Wapigakura, lakini hana taarifa za watu kupigwa risasi na kwamba anachojua ni risasi hizo kupigwa hewani na hivyo hazijajeruhi mtu.
 
“Taarifa nilizonazo ni kwamba polisi wamerusha risasi juu kwa bahati mbaya wakati wakijitayarisha kuweka sawa vifaa vyao,” alisema Kamanda Saad.
Hata hivyo, Kamanda Saad aliahidi polisi kufanya upelelezi wa kina ili kujua ni kina nani wanahusika na urushaji wa risasi hizo ambazo zimewajeruhi wananchi waliokuwepo katika eneo hilo la uandikishaji wapigakura.
Majeruhi wao walipelekwa Hospitali ya Al Rahma na kupatiwa matibabu na habari zinasema hali ya mmoja wao si nzuri na amehamishiwa Hospitali ya Mnazi Mmoja kwa matibabu zaidi.
Wakati huohuo, kikao baina ya ZEC, vyama vya siasa na wadau kilichokuwa kinafanyika jana kisiwani hapa, kilivunjika jana baada ya tume kushindwa kuwasilisha ripoti ya mgawanyo mpya wa majimbo ya uchaguzi.
Uchaguzi Mkuu umepangwa kufanyika Oktoba 25, lakini hadi sasa ZEC haijaweza kutangaza majimbo mapya, jambo lililozua mzozo kwenye kikao hicho kilichofanyika Hoteli ya Bwawani. Kikao hicho kilivujika baada ya mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salum Jecha kumaliza kutoa utangulizi kuhusu hatua zilizofikiwa katika kazi ya kutayarisha mipaka ya majimbo. Alisema kimsingi ZEC tayari imeshamaliza kazi ya kufanya mapitio ya mipaka ya majimbo ya Zanzibar na kwamba wanatarajia kutoa taarifa rasmi wiki ijayo na kuwataka wadau wa uchaguzi kuendelea kuwa na subira wakati wakikamilisha kazi hiyo.
Jecha alisema kwamba kazi ya kupitia mipaka ya majimbo ilianza kufanyika Juni 9 mwaka jana na kuwapa nafasi wadau wa uchaguzi kutoa maoni yao na hatua iliyobakia ni kutangaza mipaka ya majimbo.
Hata hivyo, mwenyekiti wa chama cha AFP, Said Soud alisema kwamba anashangazwa na ZEC kushindwa kukamilisha kwa wakati mwafaka kazi hiyo na badala yake kuendelea kutoa ahadi.
“Wakati umefika wa kumshauri Rais wa Zanzibar kuvunja uongozi wa ZEC kwa sababu wanaonekana bado wanavutana na ndiyo maana wanapiga danadana katika kutoa taarifa ya ugawaji wa mipaka ya majimbo ya uchaguzi ya Zanzibar,” alisema Soud
Mwakilishi wa CCM, Rashid Ali alisema kitendo cha ZEC kuendelea kuchechemea kutoa taarifa ya mabadiliko ya mipaka kimeendelea kuathiri vyama vya siasa kwa wagombea kushindwa kuanza kufanya matayarisho ya wagombea ubunge na uwakilishi katika majimbo ya Unguja na Pemba.
“Kama majimbo ya uchaguzi ni ya wananchi, kwa nini ZEC mnashindwa kufanya kazi ya kupitia majimbo kwa muda muafaka wakati nyie ndiyo wasimamizi wa uchaguzi?” alihoji.
Mkurugenzi wa uenezi na mawasiliano ya umma wa CUF, Ismail Jussa Ladhu alisema wameshachoshwa kudanganywa na ZEC kuhusu taarifa ya mapitio ya mipaka ya majimbo ya uchaguzi, akielezea kuwa kitendo hicho ni usanii.
Alisema kwamba ZEC walitoa ahadi ya kutoa taarifa ya mipaka ya majimbo ifikapo Machi mwaka Huu, lakini walishindwa na kuendelea kutoa ahadi nyigine bila ya utekelezaji wake kuonekana, jambo ambalo halionyeshi umakini wa utendaji kazi wa tume hiyo.
 
Akizungumzia mkasa huo katibu mkuu wa Tadea alisema kwamba inasikitisha muda wa uchaguzi umekaribia lakini hadi sasa hawajui mgawanyo wa majimbo.
Miongoni mwa wadau waliyoshiriki Kikao hicho ni vyama vya siasa, na asasi za kiraia, vikosi vya ulinzi na taasisi za Serikali

Safal Group Jobs - Tanzanians - July 2015


Safal Group is continuously seeking outstanding calibre individuals to join their team – individuals with drive, passion and integrity to ensure we optimally service our customer needs.  If you are a Junior or Senior Marketing Manager, Product Manager, Brand Manager or Channel Manager and are looking for a new and challenging opportunity, we will offer you not only a job but a career.
 
Our presence across a number of African countries offers a wealth of opportunities for applying your skills and experience, and we will support your professional development every step of the way.
We are currently seeking marketing Individuals in each African country where Safal Group has a presence:-
 
Kenya
South Africa
Ethiopia
Tanzania
Uganda
Rwanda
Burundi
Malawi
Mozambique
Zambia
Angola
Desired Skills and Experience
Qualifications Required:
Undergraduate Degree in Marketing
Experience Required:
Minimum of 5 - 7 years experience in a similar role

FOR APPLICATION CLICK HERE

Barclays Bank Jobs - Tanzanians


 
Tokeo la picha la BARCLAYS
With a global footprint of operations in 57 countries around the world and 140 000 employees, working for Barclays Africa not just offers you a career in Africa, but also connects you to our other international offices.
With a history of doing business in Africa for over a hundred years, we have a presence across 14 countries in Africa. A career at Barclays promises opportunity and challenge – an opportunity to be part of an organisation that is changing the future of banking, and the challenge to drive the change and lead us into the future.
 

FOR APPLICATION AND OTHER INFORMATION; CLICK HERE

Wanachama wawili CUF wapigwa risasi kwenye uandikishaji kwa BVR


 
 
Zanzibar: Kuna habari zinasema kwamba Wanachama wawili wa CUF  wamepigwa Risasi na watu wasiofahamika waliojifunika sura  zao  wakati wa kuandikisha wakupiga kura Makunduchi, Zanzibar.

UREMBO: VYAKULA AMBAVYO VINAWEZA KUHARIBU RANGI NYEUPE YA MENO YAKO

 


 
Na Mchambuzi wa Mambo ya Urembo

  
Kama wewe ni mtu unayezingatia sana masuala ya urembo, umakini  ni suala la msingi sana hasa katka kuchagua aina ya vyakula. Uchaguzi huo haubakii kwenye kuangalia vyakula visivyonenepesha bali ata vyakula ambavyo vinaweza vikakuaribia muonekano wa meno yako.
 




"Nafikiri umeshawahi kukumbana na mtu mmoja au wawili au zaidi ambao hukuweza kuyaangalia meno yao mara mbili. "







Leo hii nimeamua kukupa "bonus topic " ya mambo yanayohusiana na meno. Kama tunavyojua meno ni sehemu muhimu sana ya urembo na muonekano, na ni kati ya kitu kinachokuonekana cha kwanza kabisa pale uapokutana na mtu kwa mara ya kwanza.
Wataalamu wa urembo wa meno kutoka jiji la New York nchini Marekani wamekuja na list ya vyakula ambavyo matumizi yake yanaweza yakasababisha kupotea kwa rangi na mng'ao wa meno yako na jinsi gani utaweza kudumisha mng'ao wa meno yako.
 
 

1. Kahawa

Kama wewe ni mpenzi wa kahawa hii inakuhusu. Wataalamu wanakushauri kutotumia kahawa plain badala yake uchanganye na maziwa ili kupoteza rangi ya kahawa. Hii nikwa sababu ukinywa kahawa " plain" rangi nyeusi ya kahawa inatabia ya kuchafua meno. Siyo hilo tu la kuchafua meno vile vile kahawa huwa na tabia ya kukausha mate hivyo ni kiasi kidogo sana cha mate kitabaki kwaajili ya kuondoa madoa yatakayo baki kwenye meno. Haya anayaongea Dr. Nancy Rosen, daktariwa meno kutoka Jiji la New York.

 

2. Vyakula vilivyosindikwa vyenye wanga

Vyakula vyenye wanga kama vile crakers, cookies, white bread (mikate ya ngano iliyokobolewa) na yakula vingine vilivyosindikwa havitachafua meno yako pekeyake bali husababisha ata meno kutoboka. Hii ni kwa sababu mara nyingi "snaks" zinakuaga na kiwango kikubwa cha sukari, na iwapo sukari hii itabaki kwenye meno kwa muda mrefu bakteria waliopo kwenye kinywa huitumia sukari hii na kutengeneza asidi ambayo husababisha meno kutoboka. Anasema Dr. Nancy Rosen

 

3. Red Wine (Wine nyekundu)

Rangi na asidi iliyopo kwenye wine nyekundu husababisha kulika kwa sehemu ya nje ya meno kitaalamu inaitwa "enamel erosion". Chenga chenga zilizopo kwenye wine nyekundu pia huchangia kwa kiasi kikubwa kuchafuka kwa meno, kwani hupenyeza na kuingia kwenye nafasi za meno. Anaelezea daktari wa meno Dr.Gregg Lituchy kutoka Lowenberg na Lituchy.
 
 
image

4.  Sosi ya nyanya (Tomato Sauce)

Sosi ya nyanya ni kati ya vyakula ambavyo vina kiwango kikubwa cha asidi ambayo ndiyo chanzo kikubwa cha meno kuchafuka na kulika. Badala ya kutumia tomato sosi unashauriwa kutumia salads au kachumbari ili kuyalinda meno yakokuzuia yasichafuke
 
 
 
 

5. Chai

Majani ya chai yana asidi inayoitwa "tannic acid". Asidi hii inayotokana na mimea husababisha kwa kiwango kikubwa kuchafuka kwa meno hasa hasa katika sehemu ya nje. Unashauriwa kutumia green tea zaidi mbayo inahali ya alkali kuliko "black tea" ambayo inakiwango kikubwa cha asidi.
 
 
 
 
 

6. Achali 

Achali au kwa lugha ya kigeni (pickle) ni kati ya vyakula vyenye asidi nyingi. Kama tulivyoona vyakula vingine asidi ndiyo adui mkubwa wa meno kwani husababisha meno kulika na kuchafuka. Hivyo kama wewe ni mpenzi sana wa achali unashauriwa kupunguza matumizi yake na kuhakikisha unasafisha meno yako mara baaada ya kula achali. Kitu chamuhimu cha kuzingatia ni kwamba "usitumie dawa ya meno na mswaki, mara baada ya kula vyakula vyenye asidi au lugha ya kiswahili tindikali nyingi kwani kwa kitendo hichi unaweza ukasababisha kulika kwa sehemu ya nje ya meno, unashauriwa kusukutua kwa maji safi peke yake inatosha au subiri kwa saa moja kama unataka kutumia mswaki"
 
 

7. Zabibu na Berries

Zabibu nazo husababisha kuchafuka kwa meno kwa kiasi kikubwa. Zabibu na berries nazo huwa na kiwango kikubwa cha tindikali ambayo husababisha kuchafuka na kulika kwa meno
 
 
 
 
 
 

 

Hitimisho

 
Wataalamu wa meno na kinywa wanashauri matumizi ya mirija "straw" katika unywaji wa vinywaji vyenye asidi/ tindikali na rangi . Hii itasaidia katika kuyaweka meno mbali na vimiminika.
 
 

 

"JUMA PILI NJEMA"

 

UKISTAAJABU YA MUSA, HAUTAYAONA YA KWENYE SWIMMING POOL

 
 
Na. Mwandishi wetu wa Mazingira
 

Utangulizi 

Mara nyingi watu huwa wanavutiwa sana na maji ya bluu yanayong'aa kwenye swimming pool. Lakini unafahamu ni kitu gani unakipata unapoamua kuyasogelea na ku-dive kwenye hizo swimming pool?
 
Duniani kuna watu wa kila aina. Kuna watu wengine huwa wanapenda kujaribu na kuona nini kitatokea baada ya hapo. Na kati ya hawa wanaopenda kujaribu kuna waungwana na wasiokuwa waungwana.
 
Labda tujiulize katika kundi hili la watu wanaopenda kujaribu wasiokuwa waungwana, hakuna hata mmoja ambaye ataamua kujaribu ku-jisaidia haja ndogo au hata kubwa akiwa ndani ya swimming pool?

 "Nakuachia hilo swali ulijibu mwenyewe"
 

Binafsi mimi huwa sipendi kuogelea kwenye swimming pool, hata kama nitaonekana mshamba potelea pote. Nakumbuka kuna siku moja nilikua Mkoani Manyara kwenye sehemu moja maarufu. Kama unavyofahamu mkoa wa Manyara ni mkoa ambao bado ni mpya, hivyo sehemu za starehe ni chache sana. Kwahiyo hiyo sehemu tuliyoeda ndiyo sehemu ambayo ilikua na swimming pool na ndo watu wengi hupenda kwenda hapo. Kwakweli kwa jinsi nilivyoiona ile swimming pool na watu walivyokuwa wengi, nilijionea huruma afya yangu ingawa nilionekana mshamba mbele ya "washikaji" . Nahili ndilo limenifanya niandike makala hii ya leo ili walao niwape uelewa WA-TZ wenzangu.


"Declaimer: Hapa siyo Manyara tafadhali bali nimeonyesha jinsi gani swimming pool zinaweza kujaza watu wengi na hivyo kuona ni jinsi gani watu wanajihatarisha"
Nataka tuongelee "REALFACTS". Unajua ni kwahali gani unajihatarisha unapoenda kuogelea kwenye hizo swimming pool? Je, unajua ni kitu gani hasa kinapatikana kwenye hizo swimming pool. Embu twende pamoja;
 
Watu wengi sana huwa wanaamini kwamba maji ya kwenye swimming-pool ni safi na salama kwa kuwa yamewekewa Chlorine. Wazungu wanasema " sterile". Ukweli ni kwamba hii siyo kweli hata kidogo. Maji ya kwenye swimming pool SIYO MASAFI NA SALAMA, yanaweza kuwa masafi na salama iwapo hakuna mtu aliye ingia kwenye hiyo swimming pool. Narudia tena kwa herufi kubwa "YANAWEZA KUWA SAFI NA SALAMA IWAPO HAKUNA MTU ALIYEINGIA AU KU-DIVE KWENYE HIYO SWIMMING POOL"
 
 Katika mahojiano Bwana Thomas Lachocki, PhD kutoka National Swimming Pool Foundation anasema "Mtu anapoingia kwenye swimming pool maji hayo hayatakua tena safi na salama kama watu wanavyofikiri kwa sababu kuna bakteria hatari wanaoweza kuingizwa na binadamu kwenye swimming pool" . Bakteria hao na vijidudu wengine kutoka kwenye miili ya watu, wanauwezo mkubwa wa kuhimili chlorine iliyopo kwenye maji ya kwenye swimming pool.
 
Bwana  Lachocki anaendelea  kusema kwamba Bacteria watokao kwenye mkojo ni hatari zaidi, na ndiyo maana waogeleaji wengi huwashwa na macho nasehemu zingine za mwili pamoja na machoyao kuwa mekundu. Kuwashwa huku hakusababishwi na chlorine peke yake bali hutokana na " reactions" kati ya mkojo na chlorine. Kuna wengine huwa wanajidanganya kwa kunusa maji ya kwenye swimming pool.

Wengi hujipa matumaini kwa kusikia harufu kali ya maji. Ukweli ni kwamba ile harufu kali wakati mwingine husababishwa na " reaction " kati ya Klorini, mikojo, majasho, kinyesi na hata uchafu mwingine kutoka katika miili ya waogeleaji. Ndiyo maana wengine hupata hadi mafua pamoja na kikohozi wakitoka kwenye swimming pool.

"Upo hapo ?"   


Bingwa wa kuogelewa wa Olimpic wa Marekani anayejulikana kwa jina la Michael Phelps amekiri kwamba yeye na waogeleaji wenzake hwa wana-jisaiadia haja ndogo (hukojoa) ndani ya swimming pool kwa sababu anaamini kwamba klorini huua vijidudu.
 
" Kwahiyo ujinga huu unaonekana hufanywa na watu wengi, ata wazungu, kama ulikua haufahamu nafikiri sasa hivi upo katika position ya kuwashauri wengine hata huyo Michael Phelps kwani yeye ndo nani?"

 
 
Chlorine inapokutana na mkojo na uchafu mwingine, hupoteza uwezo wake wa kupambana na bacteria na vijidudu wengine. Kwahiyo chlorine inafanya kazi vizuri ikiwa yenyewe peke yake, uchafuzi wowote huifanya chlorine kupoteza nguvu yake kwani chlorine itaanza " ku-react "na uchafu na kuacha vijidudu na bacteria wakipeta.
 
Watafiti kutoka Kituo cha kuzuia na kupambana na maradhi (Centre for Disease Control and Prevention- CDC) wanasema kwamba tafiti zao zinaonyesha kwamba kwa wastani mtu mmoja hutoa  kwenye swimming pool kiasi cha;
  • 0.14 gram za " kinyesi"
  • kikombe kimoja cha mkojo
  • kiasi kikubwa cha jasho
  • na mamilioni ya vijidudu wakiwamo bakteria.


Watoto wadogo hutoa gramu 10 za kinyesi kwenye swimming pool. Kama watoto 1000 wataingia kwenye swimming pool, hii inamaana 10,000 grams za kinyesi zitatoka kwenye miili yao kwenda kwenye swimming pool.
 
Utafiti huu unaonyesha kwamba kwenye swimming pool siyo sehemu salama kabisa ya kuogelea na kufuraia kama wengi wafanyavyo, kwani kuna wenzangu hudiriki hata kuyanywa maji ya kwenye swimming pool wanapokua wanaogelea

    Hatari zingine

Maji ya kwenye swimming pool yanaweza kubeba vijidudu vinavyosababisha magonjwa kama vile E. coli na legionella." E. coli ndiyo chanzo kikubwa cha typhoid, kwa hiyo kama wewe ni mpenzi wa kuogelea usishangae kama unaugua typhoid za mara kwa mara"
 
Chlorine inaweza kuviua hivi vijidudu, lakini iwapo vitaingia mdodomi vikiwa havijafa ata kwa kiasi kidogo vinaweza vikakuletea maradhi.
 
Unatakiwa kufahamu kwamba vijidudu vinavyopatikana kwenye kinyesi cha mtu anaye "endesha" haviwezi kuuliwa na chlorine ata vikikaa kwenye swimming pool kwa siku 10.
 
Mwaka 2012 watafiti waliwachunguza waogeleaji 69 waliokuwa wanaumwa magonjwa yatokanayo na maji machafu " water borne diseases". Kati ya waogeleaji 69 nusu yao walipatikana na walipatikana na vijidudu visivyoathiriwa na chlorine.

Ushauri

Watafiti kutoka (Centre for Disease Control and Prevention-CDC) wanashauri maji ya kwenye swimming pool yawe yanaangaliwa mara kwa mara kiasi cha chlorine na pH level yake kwani vijidudu wengi husababisha kupungua kwa kiwango cha chlorine.
 
" Sijajua swimming pool zetu huwa zinachekiwa mara ngapi, au ndo asubuhi mpaka jioni au ata kesho yake, kwanza sidhani ata kama wana vipimo. Naomba uchukue hatua siku moja uwaulize kama wana rekodi ya majibu ya kiwango cha klorini kilichopo au kwa kwa lugha ya kiingereza- Chlorine Inspection and Testing Results nafikiri jibu lao litakufanya uzimie"
 
Kwa muogeleaji unashauriwa kuoga kabla ya kuingia kwenye swimming pool, ma kuhakikisha hauogelei iwapo unahisi unaumwa.
 
"Sijajua ni wangapi wenye moyo huo wa kuoga kabla ya kuogelea kwani wengi wetu huona swimming pool kama ndiyo sehemu ya kuogea"

Ushauri mwingine wa kitaalamu ni kama ufuatao;

  • Epuka kuacha maji ya kwenye swimming pool kuingia mdomoni mwako na kuyameza.
  • Usikojoe kwenye swimming pool kwani utahatarisha afya yako na ya wenzako
  • Usikae sana kwenye swimming pool, kumbuka kupumzika walao kila baada ya saa moja na kuoga . " Najua hili ni suala gumu kwa wenzangu mliolipia kiingilio cha kwenye swimming pool"
  • Kujifuta maji mara kwa mara na hakikisha taulo zinabadilishwa mara kwa mara
  • Chagua sehemu ya kwenda kuogelea, atleast hiyo sehemu iwe na historia nzuri ya usafi na kuyafanyia vipimo maji yao mara kwa mara.
 

Hitimisho

Waswahili wanasema jifunze uelimike, tafiti mbalimbali zinaonyesha kwamba "Public Swimming Pools" siyo sehemu salama kiafya. Nimeandika makala hii ili kukuonyesha hali halisi ya kile  kilichopoo kwenye swimming pool ukweli ambao pengine usingeupata.  Wengi wetu huwa tunajidanganya na chlorine (Klorini)  inayowekwa kwenye maji ya kwenye swimming pool. Kwakuwa nimeshakuelimisha ni jukumu lako kufanya maamuzi sahihi katika kuilinda afya yako.