Thursday, July 2, 2015

NJIA ZA HARAKA KUGUNDUA ASALI ILIYOCHAKACHULIWA

Na. Emanuel

Utangulizi

Asali ni zao au bidhaa linalotokana na nyuki. Ili nyuki waweze kuzalisha asali wanahitaji malighafi kama vile 'nectar" inayotokana na maua pamoja na maji. Wakati mwingine nyuki hutumia viambata vinavyotokana na majimaji miti " plant secretions". Nyuki anaweza kutembea hadi kilometa tano kutafuta maji na nekta kwa ajili ya kutengenezea asali.

Je, Unafahamu kwanini nyuki huzalisha asali?

Nyuki huzalisha asali  kwa lengo la kuweka akiba yake ya chakula kwa ajili ya matumizi ya baadae, hasa wakati wa uhaba wa chakula kama vile msimu ambao hauna maua ya kutosha ama kiangazi.

Faida za asali

Asali inafaida mbalimbali za kiuchumi na kiafya. Asali inakiwango kikubwa cha sukari "Carbohydrate' ambayo husaidia kuipa miili nguvu. Vilevile asali ina kiwango kikubwa cha madini, protini, vitamin n.k.
Katika sehemu nyingi duniani asali hutumika zaidi katika matibabu zaidi ata ya matumizi y chakula.
Asali vilevile hutumika kama chanzo cha sukari katika bidhaa mbalimbali kama vile wine na bia. Wakati mwingine asali hutumika kama malighafi katika kutengeneza bidhaa zingine kama vile vifungua kinywa, mikate n.k
  •   Aina za asali

 Kuna aina nyingi sana za asali. Aina hizo zinatokana na sababu mbali mbali kama vile;
1. Aina kutokana na chanzo cha asali
mfano:
> Asali inayotokana na nekta za maua (Blossom Honey)
>Asali zinazotokana na aina moja ya maua (Mono-floral Honey) mfano asali zinazotokana na maua ya alizeti na
 >Asali zinazotokana na mchanganyiko wa maua (Multi-floral Honey). Asali zinazotokana na maua ya aina moja huuzwa kwa bei ghali zaidi ya asali zinazotokana na maua ya aina nyingi-polyfloral.
2. Aina kutokana na matumizi ya asali- mfano: Asali ya mezani na asali za viwandani n.k
  • Njia za kujua asali iliyochakachuliwa 

"Nafahamu wewe ni mnunuaji mzuri sana wa asali. Umeshawahi kujiuliza asali unayonunua ni asali kweli 100% au kuna wajanja wamefanya mambo yao wanayoyafahamu?"

 Uchakachuaji wa asali hufanyika kwa lengo la kufanya udanganyifu kwa mnunuzi na kumuongezea faida muuzaji. Iwapo uchakachuaji utafanyika vizuri bila mnunuaji kutambua, muuzaji anaweza akapata faida zaidi ya mara mbili. 

Uchakachuaji unafanyikaje?

 Uchakachaji huweza kufanyika katika hatua mbalimbali kwenye mashamba au kwa wauzaji (Vendors).
"Najua wewe ni mnunuaji mzuri sana wa asali pale stendi ya singida, Dodoma n.k. "  
Mara nyingi uchakachuaji hufanyika kwa njia kuu tatu;
    1. Kuongeza sukari guru
    2. Kuongeza sukari iliyounguzwa/ Caramel"
    3. Kuongeza maji
     

Utajuaje kwamba asali imechakachuliwa?

Iwapo uchakachuaji wa aina hii utafanyikan utafanyika zipo njia tano rahisi za  kugundua udanganyifu huu. Njia hizo ni hizi zifuatazo;
 1. Mimina asali kidogo katika chupa ya maji safi.
 Iwapo maji yatachafuka (kuchukua rangi ya brown au rangi ya asali) ujue asali hiyo inakitu kingine imefanyiwa mambo. Asali ina uwezo mdogo sana wa kuyeyuka katika maji, kwa hiyo iwapo maji yatachafuka ujue kwamba asali hiyo imechakachuliwa.
2. Mwaga asali chini kwenye mchanga.
Katika jaribio hili iwapo mchanga utalowana, ujue asali hilo imefanyiwa maujanja. Asali halisi 100% haiwezi kulowanisha mchanga.
3. Weka asali kwenye karatasi nyeupe.
Katika jaribio hili, iwapo asali itakua imechakachuliwa kwa kuongeza maji au sukari italowanisha karatasi kwa haraka. Asali halisia 100% haiwezi lowanisha karatasi kwa haraka, itachukua mda mrefu kulowanisha karatasi.
4. Weka asali kwenye kijiko na uimwage taratibu
Kwa jaribio hili utaweza kuijua asali ambayo haijachakachuliwa itamwagika bila kukatika, wazungu wanasema " Ze honey will form a single line". Ukiona asali yako inakatika na kufanya kama matone hivi ujue umeuziwa asali iliyowekwa maji.
5. Kuchovya asali kwenye kitambaa cha pamba na kukiwasha kwa njiti kiberiti.
Iwapo kitambaa kitawaka asali hiyo haijachakachuliwa. Kama imewekewa maji kitambaa hakitawaka.
  • Hitimisho.

Kuna njia nyingi za kimaabara ambazo zinaweza kufanyika kujua kama imechakachuliwa, njia hizo tano nilizo kuelekeza ni hatua za awali na za mwanzo kabisa unao weza kuzifanya kabla haujashikishwa asali feki.


Tume Ya Uchaguzi Yatangaza Kuanza Uandikishaji BVR Dar es Salaam na Pwani


Dar es salaam: Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura kwa teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR) lililoahirishwa katika jiji la Dar es salaam na mkoa wa Pwani hivi karibuni sasa litafanyika kuanzia  Julai 7-20 kwa mkoa wa Pwani na Julai 16- 25 kwa jiji la Dar es salaam. 
Uboreshaji wa Daftari hilo kwa jiji la Dar es salaam na Mkoa wa Pwani uliahirishwa kutokana na kuchelewa kwa vifaa vya uboreshaji kutoka mikoani ambavyo vilipelekwa ili kuongeza ufanisi kutokana na maeneo hayo kuwa na idadi kubwa ya watu wenye sifa ya kuandikishwa kuwa Wapiga Kura.

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Julius Mallaba amewataka wananchi wote wa mikoa hiyo kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vya uandikishaji vitakavyokuwa kwenye Vijiji, Vitongoji na Mitaa ili kujiandikisha  waweze kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowataka katika Uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba Mwaka huu.

Amewataja watakaohusika na zoezi hili kuwa ni watu wote waliotimiza umri wa Miaka 18 na kuendelea na wale watakaotimiza Miaka 18 ifikapo mwezi Oktoba Mwaka huu.

Wengine ni waliojiandikisha awali kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la zamani ili kuhuisha taarifa zao na kupata kadi mpya za kupigia kura. Aidha Mallaba amewataja wengine wenye sifa ya kujiandikisha kuwa ni wale wote wenye sifa za kujiandikisha lakini hawajawahi kujiandikisha kwenye Daftari hilo.

Amesema wale wote wenye Kadi za kupigia Kura za zamani wanatakiwa kwenda na Kadi zao ili kurahisisha uchukuaji wa taarifa zao na kadi hizo zitarudishwa NEC na watapata vitambulisho vipya.  Wananchi wanatakiwa kujiandikisha katika Vituo vilivyopo ndani ya Kata zao ili kuweza kupata fursa ya kumchagua Diwani, Mbunge na Rais.

Mkurugenzi huyo ametoa wito kwa wananchi wa mikoa hiyo kuhakikisha wanajiandikisha kwani bila kufanya hivyo hawataweza kupiga Kura wakati wa Uchaguzi Mkuu. Vituo vya kujiandikisha vitafunguliwa kila siku kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa ifikapo saa 12:00 jioni

NAFASI YA KAZI

Public Relations Officer II-1 POST

Duties and Responsibilities
To collect and compile news for the institute’s newsletter
To collect and compiled information which shall assist in the preparation of annual reports, booklets, speeches, prospectus
To ensure proper recording and filing of press cuttings for public relation and responses
To supervise production and distribution of promotional materials
To liaise with the mass media on press matters relating to institute of Social Work
To draft replies to general correspondences directed to the institute concerning meia
To assist and coordinate awareness activities at the institute and
To perform any other duties as may be assigned by higher authority

Qualification and Experience
Holder of a Maters Degree in Public Relations , Mass Communication , Administration/Management .
Must have at least thirteen years work experience

Remuneration
Attractive remuneration package in accordance with the Institute Salary Scale
 

Planning Officer

Planning Officer II-1 POST

Duties and Responsibilities
To assist in planning and control of development projects of the institute
To assist in coordination and supervision of implementation of institutes’ strategic action plan
To assist in identifying internally generated income activities
To assist in the formulation and coordination of the institute’ pals and strategies based upon priorities for resources allocation to various functional programmes
To assist in preparation of basic statistical and management planning reports and
To prepare short term and long term development plans
To deal with all issues related to planning and budgeting
To keep statistics and reports on the performance of the institute and
To perform any other duties as may be assigned by higher authority

Qualification and Experience
Holder of a bachelor Degree in Economics , Educational Planning , Management , Statistics or any other related field

Remuneration
Attractive remuneration package in accordance with the institute salary scale
 

Electrical Technician

Electrical Technician II-1 post

Duties and Responsibilities
To perform daily works of installation and fixing broken units in the system
To carry out minor repair work
To ensure electrical systems are operating properly
To identify and report on areas that need rehabilitation in the electrical system including the quantity of material required for repair of works
To identify likely defects that might cause damage in the electrical
To ensure maintenance of electrical systems of office , staff and hostel buildings
To ensure safe custody of tools and equipment and
To perform any duty as assigned by higher authority
Qualification and Experience
Holder of form IV certificate who has successfully completed Full Technician Course Or holder of trade test I certificate in related field from any recognized any recognized institution

Remuneration
Attractive remuneration package in accordance with the institute salary scale

Legal Officer II

Duties and Responsibilities
To compile evidence relevant for court cases
To advice on aspects regarding contract obligations and any other legal obligations
To inform the charges in law or new legislation affecting the institute
To prepare and reviews proposed contracts , leases , loan agreements and other legal documents in order to safeguard
To handle all legal matters of the institute
To represent ISW and prepare briefs in all legal proceedings of the institute
To prepare legal drafts and provides legal advice and
To perform legal drafts and provides legal advice and
To perform any other duties as may be assigned by higher authority

Qualification and Experience
Holder of LLB Degree plus one year internship or has attended Law School of Tanzania

Admission Officer II -1 post

Duties and Responsibilities
Be responsible for implementing of the institute admission procedures
To issue joining instructions to new selected students
To liaise with the academic departments to ensure that there is a proper records of admitted students
To prepare students directory and undertake students statistics
To process institutes applications for admission
To keep proper records of all students admission matters and
To perform any other duties as may be assigned by the higher authority

Qualification and Experience
Holder of a bachelor Degree or advanced diploma in social sciences disciplines from the recognized institution

Remuneration
Attractive remuneration package in accordance with the government salary scale

Tutorial Assistant-x 4 posts
One in Human Resources , one in Labour studies and two in Social Work field

Duties and Responsibilities
To assist in conducting seminars and tutorials under close supervision
Prepare materials for tutorial exercises
Assist in teaching in the Certificate Course
Conduct research under close supervision
Carry out consultancy and service job assignments under close supervision
Any other duties as may be assigned by the supervisor

Remuneration
Attractive remuneration package in accordance with the institute salary scales
Tutorial Assistant-x 4 posts
One in Human Resources , one in Labour studies and two in Social Work field

Duties and Responsibilities
To assist in conducting seminars and tutorials under close supervision
Prepare materials for tutorial exercises
Assist in teaching in the Certificate Course
Conduct research under close supervision
Carry out consultancy and service job assignments under close supervision
Any other duties as may be assigned by the supervisor

Remuneration
Attractive remuneration package in accordance with the institute salary scales
 
APPLICATION INSTRUCTIONS:
Interested Candidates should apply in confidence , enclosing certified copies of academic transcript and certificates( Including birth certificate), one current passport size photograph and a detailed CV with at least two referees.The application letter should be handwritten and reach the undersigned within two weeks after the date of the first advertisement.

Only shortlisted will be contacted and called for the interview through their respective employers
Rector
Institute of Social Work
P.O B.O.X 3375
DAR ES SALAAM
 Source: Kazibongo

Watano wanashikiliwa na Polisi kutokana na wizi wa Milioni 200, uliotokea katika Benki ya NMB Mkuranga

 
Watu watano, akiwemo mfanyakazi wa NMB wanashikiliwa na polisi kutokana na kuhusishwa na wizi wa mil 200 katika benki ya NMB tawi la Mkuranga mkoa wa Pwani.
 
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Pwani-CP, Jafari Ibrahim, watu wane kati yao ni walinzi waliokuwa wanafanya kazi katika kampuni binafsi ya ulinzi iliyopewa jukumu la kusafirisha fedha kutoka Dar es salaam kwenda Mkuranga-Pwani.

 Kamanda wa poilisi ameongeza na kusema kwamba, mtuhumiwa mwingine aliyekamatwa ni mfanyakazi wa NMB ambaye jina lake na cheo chake vinahifadhiwa, na anaendelea kuhojiwa na polisi.

 Majambazi watatu waliokuwa na silaha aina ya SMG walivamia na kuua polisi mmoja na kujeruhi watu wawili katika tukio lililotokea tare 26 mwezi wa sita, kaba ya kupora pesa zaidi ya mil 200 katika benki ya NMB tawi la Mkuranga. Tukio hilo lilitokea mda mchache baada ya kuwasili kwa fedha kutoka Dar es salaam. Katika siku ya tukio, majambazi walimuua afisa polisi mmoja ambaye hakuwa katika zamu siku ya tukio lakini alikua kwenye benki hiyo ambaye alikua anasubiri shifti ya usiku. Watu wengine wawili walijeruhiwa na kuwahishwa katika hospitali . Mpka sasa majeruhiwa wamesharuhusiwa.

JUISI YA MIWA INAWEZA KUSAIDIA KUBORESHA AFYA YAKO

Na. Emanuel Cosmas
                                                                         

Utangulizi

Unapopita maeneo mengi ya mijini na pembezoni wa miji utakutana na wafanya biashara wa miwa wanaouza miwa na wanaouza juice ya miwa. Wengi hununua juisi ya miwa kwa kuwa hufuraia utamu wake. Lakini umeshajiuliza juisi ya miwa inafaida gani kiafya?

Faida za kiafya za juisi ya miwa

Kunafaida nyingi za juisi ya miwa. Baadhi ya faida hizo ni kama zifuatazo;



1. Uwezo wa kuipa miili nguvu kwa haraka "instant kick of energy"

Juisi ya miwa inauwezo mkubwa wa kuipatia miili nguvu kwa haraka na kukata kiu ya maji. Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari "sucrose" ambayo kazi yake kuu ni kutengeneza nguvu mwilini. Kwahiyo wakati mwingine ukiwa na nguvu au uchovu, badala ya kunywa vinywaji vya viwandani tafuta juisi ya miwa. 
  

2. Juisi ya miwa ni nzuri kwa watu wenye Kisukari


Ingawa jusi ya miwa ina utamu inafaa sana kwa watu wenye kisukari. Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari halisi ambayo ina uwezo mdogo wa kuzidisha kiwango cha sukari mwilini au kitaalamu inaitwa "Low Glycemic Index". Kutokana na hilo jusi ya miwa inashauriwa kutumiwa kama mbadala wa vinywaji vingine vya viwandani. Ni mhimu pia kwa watu wenye kisukari kutumia juisi hii kwa kiasi kidogo au kulingana na ushauri wa daktari.

    3. Juisi ya miwa inasaidia kupunguza matatizo ya kansa

 Juisi ya miwa ina kiwango kikubwa cha madini ya calcium, magnesium, potassium, chuma n manganese. Madini haya yana uasili wa ualkali ambao husaidia kupunguza uwezekano wa kupata kansa kama vile kansa ya Tezi dume "Prostate cancer" na kansa ya maziwa "Breast Canser"

 4. Juisi ya miwa huipatia miili  protein

Juisi ya miwa inasaidia kuongeza kiwango cha protein mwilini na ku-imarisha ufanyaji kazi wa figo.
Juisi a miwa iliyochanganywa na maji ya Nazi husaidia kupunguza maumivu hasa yanayosababishwa na maambukizi ya ngono "STDs" na kidney stones.

5. Juisi ya miwa inasaidia kupambana na maambukizi na kuimarisha kinga ya mwili.

Juisi ya miwa husaidia kulinda maini yasipate maambukizi. Hii ndo maana Ma-daktari hushauri matumizi ya juisi ya miwa kwa watu wenye ugonjwa wa Homa ya Manjano,
     

6. Juisi ya miwa husaidia kuimarisha mmeng'enyo wa chakula.

Juisi ya miwa ina kiwango kikubwa ch madini ya potassium ambayo husaidia kuimarisha mmeng'enyo wa chakula. Vilevile juisi ya miwa husaidia kuzuia maambukizi katika tumbo na utumbo. Vilevile husaidia katika kutibu matatizo ya choo kigumu au kitaalamu inaitwa "constipation".   

7. Juisi ya miwa husaidia kuzuia kuoza kwa meno

Uchunguzi unaonyesha juisi ya miwa husaidia kuzuia meo kuoza na matatizo ya kupumua kutokana na  kuwa na kiasi kikubwa cha madini. Kwa hyo kama unafikiria kwenda kwa daltari kung'arisha meno yako, kunywa juisi ya miwa mara kwa mara.

 8. Juisi ya miwa husaidia kuimarisha ngozi.

Juisi ya miwa husaidia katika kupambana na mabaka mabaka na kung'arisha ngozi. Juisi ya miwa huweza kutumika kama " face mask na scrub" kwa kuipaka kwenye ngozi na hivyo kusaidia katika kuing'arisha na kuiimarisha.

Hitimisho

juisi ya miwa inafaida nyingi mwilini, ni muhimu kuhakikisha usafi katika utengenezaji wake. Juisi ya miwa isiyokuwa salama inaweza ikawa ni chanzo kikubwa cha magonjwa ya tumbo na kuhara.
.

Polisi Yanasa Mtambo Wa Kutengeneza Bunduki



Rukwa: POLISI mkoani Rukwa imewakamata watuhumiwa 19 na silaha za aina mbalimbali zikiwemo bunduki 30, risasi 231 pamoja na mtambo wa kutengeneza bunduki za kienyeji.
 
Katika msako uliofanywa na Polisi mkoani hapa, pia waliweza kukamata nyara za Serikali yakiwemo meno, mikia miwili ya tembo na maganda mawili ya risasi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema jana mjini hapa kuwa silaha hizo zilikamatwa kutokana na operesheni ya kupambana na visa vya ujangili na uhalifu mwingine katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa huu.
Alibainisha kuwa silaha hizo zilizokamatwa zinasadikiwa kutumika katika visa vya kijangili na uhalifu mwingine ambapo baadhi ya bunduki zimegundulika kuwa zinamilikiwa kihalali.
 
Alizitaja silaha zilizokamatwa kuwa ni bunduki aina ya shotgun 8, rifle 8, magobori 4, bunduki 6 aina ya shotgun zilizotengenezwa kienyeji, risasi 5 za SMG, risasi 53 za rifle na risasi 173 za shotgun.
 
Kwa mujibu wa Kamanda Mwaruanda watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote baada ya uchunguzi wa awali wa kukamilika.

Watuhumiwa wa EPA Waachiwa Huru.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewaachia huru Kada wa CCM Rajabu Maranda na wenzake waliokuwa wanakabiliwa na kesi wizi wa Sh milioni 207 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
 
Jopo la mahakimu watatu likiongozwa na Hakimu John Utamwa, Ignas Kitusi na Eva Nkya liliwaachia washitakiwa hao baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi ya washitakiwa hao.

Mbali na Maranda washitakiwa wengine walioachiwa huru ni Farijala Hussein na waliokuwa wafanyakazi wa BoT, Ester Komu, Bosco Kimera na Imani Mwakosya.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Utamwa alisema washitakiwa waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka manne kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo BoT na wiziwa Sh milioni 207.2 wako huru kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka hayo bila kuacha shaka kama inavyotakiwa kisheria.

Alisema upande wa Jamhuri umeshindwa kuithibitishia mahakama jinsi Maranda na Farijala walighushi makubaliano ya kukusanya deni kati ya Kampuni ya General Marketing ya India kwenda Kampuni ya Rashas (T) ya Tanzania.

Katika hukumu hiyo iliyosomwa bila Mwakosya kuwepo mahakamani, Hakimu Utamwa alisema upande wa Jamhuri wameshindwa kumleta mpelelezi wa kesi hiyo ili aweze kuithibitishia Mahakama saini ambazo zinadaiwa kuwepo katika makubaliano hayo hivyo udhaifu huo hauwezi kuwatia washitakiwa hatiani.

Aliongeza kuwa, upande wa Jamhuri ulishindwa kuthibitisha shitaka la kughushi, kwa hiyo shitaka la kuwasilisha nyaraka za uongo litakuwa limekufa,kwa sababu wameshindwa kuonesha kweli nyaraka ni za kughushi.

Aidha alisemwa wameshindwa kuonesha ni jinsi gani fedha hizo zilihamishwa kama wanavyodai kuwa mchakato huo ulifanikiwa kwa sababu Maranda na Farijala walitumia nyaraka za kughushi.

“Hakuna shahidi aliyeweza kutoa ushahidi ukaenda sawa na hati ya mashitaka iliyofunguliwa mahakamani hapo dhidi ya washitakiwa,” alisema Hakimu Utamwa.

Nyaraka zinazodaiwa kughushiwa ni hati za makubaliano ya kuhamishiwa deni kutoka Kampuni ya General Marketing ya India kwenda Kampuni ya Rashas (T) ya nchini Tanzania, ambazo walizutumia na kuiba fedha hizo.

Baada ya Hukumu hiyo, Farijala alirudishwa rumande kwa sababu anatumikia kifungo cha miaka miwili jela alichohukumiwa katika kesi nyingine na Maranda aliachiwa lakini bado ataendelea kwenda mahakamani kwa kuwa anakabiliwa na kesi nyingine.
 
Ndugu na marafiki waliokuwepo katika eneo hilo la mahakama walishukuru mahakama kutoa uamuzi wa haki na kusema kweli Mungu ametenda miujiza.

Wanachama 32 kati ya 42 wamesharudisha fomu: Lowassa asema amechoka kuitwa fisadi

Dodoma. Waziri Mkuu aliyejiuzulu , dward Lowassa jana aliwataka wanaomhusisha na ufisadi kuacha mara moja kwa sababu hakuna hata chembe ya ukweli katika tuhuma hizo.
Lowassa, aliyeonekana kuzungumza kwa hisia, alisema hayo jana mara baada ya kurejesha fomu ya kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.
Mbunge huyo wa Monduli alikuwa mmoja kati ya makada tisa waliorudisha fomu jana, ikiwa ni siku moja kabla ya kuisha kwa muda uliowekwa na chama hicho. Wengine waliorejesha fomu jana ni Elidephonce Bilohe, Mwigulu Nchemba, Luhaga Mpina, Dk Hamisi Kigwangalla, Hassy Kitine, Mariki Marupu, Dk Asha Rose Migiro na Lazaro Nyalandu.
Hadi sasa, tayari wanachama 32 kati ya 42 wa CCM walioomba kuteuliwa na chama hicho kugombea urais wamerudisha fomu na kazi hiyo itahitimishwa leo.
Hakuna mtu ambaye amejitokeza hadharani kumtuhumu Lowassa kwa ufisadi, lakini tuhuma hizo zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, hasa kutokana na mbunge huyo wa Monduli kujiuzulu nafasi ya Waziri Mkuu mwaka 2008 baada ya kuibuka sakata la mkataba wa ufuaji umeme wa dharura baina ya Serikali na Kampuni ya Richmond RDC ya Marekani ambayo ilionekana haina uwezo.
Wakati huo, Lowassa alisema kwenye hotuba yake ya kujiuzulu kuwa amefanya uamuzi huo “ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji, lakini kutokubaliana na utaratibu uliotumika wa kusema uongo ndani ya Bunge kwa kumsingizia mtu.”
Akizungumza jana kwenye ofisi za makao makuu ya CCM, Lowassa alirudia wito wake wa kutaka wenye ushahidi wa tuhuma hizo wajitokeze hadharani.
“Nataka nitumie fursa hii kuwataka wale wote ambao wamekuwa wakinituhumu kwa miaka kadhaa sasa na kunihusisha na suala zima la rushwa, nawaambia waache mara moja, kwani hakuna chembe hata ya ukweli wa maneno hayo,” alisema.
“Natoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi wa tuhuma hizo za kipuuzi, autoe na aeleze kwa ushahidi rushwa yoyote inayonihusu, aseme nimechukua lini, kwa nani, kwa lipi na kiasi gani?”
Alisema yeye ni mwadilifu na anaposema atasimamia vita dhidi ya rushwa atafanya hivyo kwa vitendo bila kumuonea mtu na bila kumuonea haya yeyote.
“Ndugu wanachama wenzangu na wananchi kwa jumla, ni lazima sasa tufike mahali tuseme imetosha. Majungu yametosha, upotoshwaji umetosha, rushwa imetosha na kwa pamoja tunaweza kukomesha haya. Tutayakomesha kwa kusimamia ukweli, uadilifu, uaminifu na kutenda kwa haki,” alisema.
Ukumbi wa Whitehouse, jana ulijaa wana-CCM ambao walifika kushuhudia Lowassa akirudisha fomu tofauti na idadi iliyowahi kutokea kwa wagombea wengine kadhaa waliomtangulia. Hali hiyo ilisababisha foleni kwenye Barabara ya Mtaa wa Kuu unaopita mbele ya ofisi za CCM, na kusababisha usumbufu kwa wapita njia.
Lowassa alifika akiwa ameongozana na mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru na wenyeviti wa chama hicho wa mikoa kadhaa pamoja na wabunge.
Wabunge hao ni Andrew Chenge (Bariadi Magharibi), Peter Serukamba (Kigoma Mjini), Diana Chilolo (Viti Maalumu), Profesa Juma Kapuya (Urambo Magharibi), Mary Chitanda (Viti Maalumu), Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga na Mary Mwanjelwa (Viti Maalumu).
Baadhi ya wenyeviti wa CCM wa mikoa waliomsindikiza ni Jesca Sambatavangu kutoka Iringa, Ramadhan Madabida (Dar es Salaam), Khamis Mgeja (Shinyanga), Mgana Msindai (Singida) na Joseph Msukuma (Geita).
Wa darasa la saba atia fora
Jana, Bilohe ambaye ni mgombea pekee mwenye elimu ya darasa saba, alitia fora kwa kushangiliwa na kupigiwa vigelegele na wananchi alipofika ofisi za CCM.
Bilohe, ambaye ni mkulima kutoka mkoani Kigoma, alipokewa kwa shangwe alipofika makao makuu ya chama hicho saa nane mchana, lakini hakuwamo kwenye orodha ya makada waliokuwa wanarudisha fomu, hivyo kulazimika kusubiri wanachama wengine wawili waliokuwa kwenye orodha.
Tofauti na makada wengine ambao si maarufu katika chama hicho, Bilohe alikumbatiwa na kupepewa na watu waliokuwa eneo hilo. Akitumia staili ya kupungia mkono watu, Bilohe aliyekuwa pekee yake, alishangiliwa hata baada ya kurejesha fomu yake ya kuomba kuwania kuteuliwa na CCM kuwania urais.
Akizungumzia safari yake ya kusaka wadhamini, alisema alipokewa vizuri na wana-CCM wenzake mikoani na hakuna aliyeonekana kujali kama yeye ni mkulima.
“Hatua hii inaonyesha ukomavu wa demokrasia ndani ya CCM. Watanzania mnapaswa kujivunia kwa kuwa Mungu kawaleta duniani na kuwachagulia Taifa mtakalozaliwa na kuishi,” alisema.
Alipoulizwa changamoto alizokutana nazo wakati wa kazi hiyo ya kusaka wadhamini, Bilohe alisema kuna baadhi ya sehemu alizokwenda ambako watu walitaka wapewe fedha ili wamdhamini.
“Umejiandaaje ilikuwa ni swali gumu sana? Wengine waliomba wapewe chochote na maji ya kunywa. Nikawaambia kwenye mkoba huu sijabeba fedha. Mimi ni mkulima wa kawaida. Nyie mna jukumu la kunidhamini kama chama. Napenda kuwahakikishia kuwa hakuna pesa niliyowazawadia watu na nilipata udhamini kama chama kilivyoniagiza. Sina cha kuwalipa wote ambao waliacha kazi zao na kuja kunidhamini.”
 
Awali, Nchemba ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha, aliwataka wanaoipinga Katiba Inayopendekezwa kufuata utaratibu wa kisheria badala ya kufanya fujo kwa sababu hata kile wanachokitaka watashindwa kukitumia.
“Tufuate utaratibu tusije tukagawanyika na kupigana, tusije kudhani kuwa nchi zilizopigana vita hazikuwa na Katiba nzuri, la hasha. Tufuate utaratibu wa kisheria ili kubadilisha kwa sababu hii si Biblia wala Quran Tukufu,” alisema.
Mwigulu alisema, katika safari yake ya kukusanya wadhamini, alikutana na utayari mkubwa na kuungwa mkono na wanachama wenzake, ambao alisema wengine walijitokeza wakati mwingine kuanzia saa mbili usiku hadi hata saa sita usiku ili mradi wamdhamini.
Mpina ataka mdahalo
Mbunge wa Kisesa, Mpina alikiomba chama chake kuandaa mdahalo kwa watu 42 waliomba nafasi hiyo ili waweze kuelewa vizuri watalifanyia nini Taifa.
“Nilikuwa nakiomba chama changu kiruhusu mdahalo kwa wagombea ili kila mmoja aweze kueleza atalifanyia nini Taifa kabla ya vikao vya uamuzi (kuchuja wagombea),” alisema.
Alisema katika safari yake ya kusaka wadhamini alikwenda na watu watatu kwa kutumia gari aina ya Toyota Noah na kuwashangaa wagombea wenzake ambao walitumia mabasi na mafuso kusomba wanachama kutoka maeneo mbalimbali.
“Hakuna mgombea hata mmoja anayenitia presha na  namuomba Mungu nipite na kuingia tatu bora,” alisema Mpina, ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi, Biashara na Masoko.
Kigwangalla alia na ufisadi
kwa upande wake, Dk Kigwangalla ambaye ni Mbunge wa Nzega alisema Tanzania inahitaji mabadiliko na imechoshwa na ufisadi na kwamba akifanikiwa kuwa rais ataiongezea nguvu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ili iweze kufanya kazi.
Alisema yuko tayari kushirikiana na mgombea yeyote atakayepitishwa na chama katika vikao vyote iwapo yeye hatateuliwa.
 
Kitine akomalia rushwa
Akizungumza jana, Dk Kitine ambaye ni mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa alisema endapo atapitishwa, atakomesha rushwa ndani ya kipindi cha miaka miwili ya uongozi wake.
“Ninajua namna ya kushughulikia rushwa ambayo ni chanzo kikuu cha maovu nchini. Nitatumia miaka miwili kukomesha rushwa nchini,” alisema Kitine na kuongeza kuwa sheria ya kupambana na rushwa haitaacha mwanya kwa hakimu kutoa hukumu anayoiona yeye badala yake sheria itaainisha adhabu anayotakiwa kupata mtu atakayepatikana na hatia ya rushwa.
Marupu aonya wapambe
Baada ya kurejesha fomu, Marupu (34) ambaye ni mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu cha Mzumbe aliwataka wagombea wenzake kuwa makini na wapambe wanaowaunga mkono wasije wakakipasua chama.
“Tunapata shida sisi wagombea, tunashindwa hata kusalimiana tukionana kwa kuogopa kupigwa na wapambe. Wagombea wenyewe hawana shida, shida ipo kwa wapambe. Mtatuua jamani,” alisema.
“Kama kuna mtu anamuabudu mgombea atuachie chama chetu. CCM haitapasuka nyie ndiyo mtapasuka nyote. Kama majina yatapita kama ilivyo nitawachakaza vizuri sana.”
Alisema amechukua wadhamini pia kutoka mkoa maalumu wa vyuo vikuu wa CCM.
Nyalandu ataka umoja
Waziri huyo wa Maliasili na Utalii, aliwataka wafuasi wa CCM kuimarisha kwa vitendo umoja ndani ya chama hicho.
Alisema katika ziara yake ya kutafuta wadhamini, aligundua kuwa vitu vinavyowaunganisha kama Taifa ni vingi kuliko vinavyowatenganisha.
Aliwataka pia wagombea wenzake na Watanzania kushiriki katika kupiga vita ubaguzi wa aina zote

Wanafunzi 18,751 wakosa nafasi kidato cha tano


Dar es Salaam. Wanafunzi 18,751 waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka 2014, wamekosa nafasi ya kujiunga na shule za kidato cha tano kwa sababu mbalimbali ikiwamo ufinyu wa nafasi.
Kati ya hao, wanafunzi 479 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya ufundi huku idadi ya wanafunzi wa kike waliochaguliwa kujiunga na vyuo hivyo ikiongezeka kwa asilimia 25 kutoka wanafunzi 117 mwaka 2014 mpaka kufikia wanafunzi 147 mwaka huu.
“Baadhi ya wanafunzi wamekosa nafasi kutokana na umri mkubwa na baadhi ya watahiniwa wa kujitegemea wanakosa sifa za kuchaguliwa,” Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Kassim Majaliwa alisema hapa jana alipokuwa akitangaza kuchaguliwa kwa wanafunzi hao.
Alisema wanafunzi 55,003 sawa na asilimia 74.5 ya wanafunzi 73,754 waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano.
Majaliwa alisema kuna ongezeko la ufaulu la wanafunzi 918 mwaka huu, ikilinganishwa na wanafunzi 54,085 waliochaguliwa mwaka 2014 kujiunga na kidato cha tano.
Alisema wanafunzi waliokosa nafasi kuingia kidato cha tano watadahiliwa na Baraza la Taifa la Ufundi (Nacte) kwenye fani mbalimbali kama vile ualimu, afya, maendeleo ya jamii na kilimo.
Alisema ufaulu wa watahiniwa wa kidato cha nne mwaka 2014 kuanzia daraja la ‘distinction’ hadi ‘credit’, yaani ufaulu wa wastani (GPA) wa 5.0 hadi 1.6 ni watahiniwa 73,754 sawa na asilimia 37.4 ya wanafunzi 240,410 waliofanya mtihani huo.
Alisema uchaguzi ulifanyika kwa kufuata machaguo matano ya tahasusi (combinations) yaliyojazwa na wanafunzi kwenye fomu ya uchaguzi ‘Selform.’
Alisema mfumo wa kompyuta ulitumika katika kumpanga mwanafunzi katika uchaguzi wake wa masomo na shule kwa kuanzia na chaguo la kwanza. “Kama mwanafunzi atakuwa hana sifa katika machaguo yote aliyoomba, hupangiwa chaguo la somo alilofaulu zaidi na katika shule iliyopo karibu na wilaya yake ya makazi kulingana na tahasusi na nafasi zilizopo,” alisema Majaliwa.
Alisema wanafunzi 29,744 watajiunga na masomo ya sayansi na 25,259 watajiunga na masomo ya sanaa na biashara.
Aliwataka wanafunzi waliochaguliwa kuripoti katika shule walizopangiwa ili kuanza muhula wa kwanza wa masomo unaotarajiwa kuanza Julai 18.
“Naagiza wanafunzi wote kuripoti katika shule walizopangiwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya wiki mbili kuanzia tarehe ya mwisho ya kuripoti, nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine aliyekosa nafasi,” alisema Majaliwa ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa, Lindi.

BEI YA PETROLI YAPAA KWA SASA NI Sh2,200 KWA LITA


Dar es Salaam.


Serikali imepandisha bei ya mafuta kuanzia leo baada ya jiji la Dar es Salaam kukumbwa na uhaba wa muda wa nishati hiyo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kusitisha mauzo kusubiri kunufaika na bei mpya.
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) ilitangaza jana kuwa kuanzia leo bei ya petroli imepanda kwa Sh232 kutoka bei ya sasa ya Sh1,966. Bei ya kikomo ya petroli sasa itakuwa Sh2,198, ikiwa ni ongezeko la asilimia 11.82.
Bei ya dizeli imepanda kwa Sh261, ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.65 na hivyo bei mpya itakuwa Sh2,043 badala ya Sh1,782, wakati mafuta ya taa yamepanda kwa Sh369 sawa na asilimia 22.75.
Tangu bei ya mafuta ghafi ishuke hadi chini ya Dola 50 za Marekani kwa pipa mapema mwaka huu na kusababisha bei ya petroli kushuka hadi Sh1,652 mwezi Machi, mwenendo wa bidhaa hiyo imekuwa ni kupanda.
Hadi jana, mafuta ghafi duniani yalikuwa yanauzwa chini ya Dola 60 za Marekani kwa pipa katika soko la dunia, lakini nishati hiyo nchini imerejea kwenye bei ambayo mafuta ghafi yalikuwa yakiuzwa Dola 100 kwa pipa.
Mkurugenzi mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi aliwaambia waandishi jana kuwa mabadiliko aliyotangaza yanatokana na bei ya mafuta katika soko la dunia, pia kuendelea kudhoofika kwa thamani ya shilingi dhidi ya Dola ya Marekani pamoja na mabadiliko ya tozo za Serikali katika mafuta kuanzia Julai Mosi, 2015.
Alisema thamani ya shilingi kwa machapisho ya bei za Juni na Julai 2015, imepungua kwa Sh 175.11 dhidi ya dola ya Marekani sawa na anguko la asilimia 8.65.
“Juni mwaka huu bei za jumla petroli ziliongezeka kwa Sh232.35 kwa lita sawa na asilimia 12.49, dizeli Sh261.15 kwa lita sawa na asilimia 15.57 na mafuta ya taa Sh369.41 kwa lita sawa na asilimia 24.32,” alisema Ngamlagosi.
Pamoja na naibu waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage kutoa tamko kali bungeni kuonya wafanyabiashara dhidi ya vitendo vya kutouza mafuta, baadhi ya vituo vilikuwa havitoi huduma jana na juzi.
Ewura ilisema jana inamfuatilia mtu aliyesambaza ujumbe kwa njia ya mitandao ya kijamii kutaarifu kuwapo kwa njama za wafanyabiashara kutouza mafuta kwa siku mbili kusubiri bei mpya.
Ngamlagosi alisema Ewura imeiandikia barua Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Jeshi la Polisi kutaka wachunguze kujua ujumbe huo ili muhusika achukuliwe hatua.
“Upungufu wa mafuta uliojitokeza mkoani Musoma na kuwasababishia usumbufu wananchi tunafuatilia na tukibaini watapewa adhabu ya kulipa faini ya Sh20 milioni au kwenda jela au kufutiwa leseni ya biashara ya mafuta,” alisema Ngamlagosi.
 
Source: Mwananchi