Wednesday, June 24, 2015

WATANGAZA NIA

MKULIMA wa Kigoma anayewania kupitishwa na CCM agombee urais kwa chama hicho, Idelphonce Bilole, ametua mkoani Morogoro akiendelea kutafuta wadhamini katika mikoa 15 nchini, huku akisisitiza elimu si kigezo cha yeye kushindwa kuwania nafasi hiyo ya juu.
Bilole aliyasema hayo jana katika ofisi ya CCM Wilaya ya Morogoro ambapo alisema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kiongozi ni lazima ajue kusoma na kuandika na kwamba CCM ni chama pekee ambacho hakina ubaguzi.
Aidha, alisema mwaka 2003 alifuatwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho wakimtaka ajiandae ili aweze kuwania nafasi hiyo kwa mwaka 2005 ambapo alisema alikubali na aliandika barua ya kuomba kuteuliwa, lakini kutokana na sababu ambazo yeye hakuzifahamu barua ile ilichelewa na hivyo kuamua kuvuta subira.

No comments :

Post a Comment