Friday, July 3, 2015

Wanne hawakurejesha fomu za CCM kuwania Urais Tanzania 2015

 
Watu wanne waliochukua fomu za kuwania kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa wagombea wa kiti cha urais wametoka rasmi katika mchakato huo, baada ya kushindwa kurudisha fomu hadi muda wa mwisho ulipofika saa 10.00 alasiri ya jana.
Watu hao ni 
  1. Peter Nyalali
  2. Helen Elinewinga
  3. Anthony Chalamila
  4. Dk Muzamil Kalokola
Jumla ya wanachama 42 walijitokeza kuchukua fomu hizo.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, Rajab Luhwavi alisema zoezi la kuchukua fomu lilianza Juni 3, mwaka huu na lilitarajia kumalizika Julai 2, 2015.
“Mmoja wa wachukua fomu, Helena Elinawinga alitelekeza fomu hizo kwa mmoja wa maofisa wa CCM baada ya kufika kuomba ushauri huku akitaka kupewa kwanza elimu ya siasa kabla ya kuanza kutafuta wadhamini” 
Luhwavi alisema hatua itakayofuata ni mchakato wa vikao vya chama kuanzia Jumanne wiki ijayo.

 

No comments :

Post a Comment