Sunday, June 28, 2015

UNAMFAHAMU KIUMBE MWENYE FURAHA KULIKO WOTE DUNIANI?

Kwa muhibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Programu za mazingira (United Nations Environment Programme -UNEP) kuna aina zipatazo million nane, laki saba za viumbe waliopo  Duniani. Kati yao wanyama wapo wa aina million 7.77, Mimea ipo ya aina 298,000, Fungus wapo wa aina 611,000 na Protozoa wapatao 36,400.

 
 
 
Kati ya viumbe wote hao kuna mnyama mdogo anayepatikana nchini Australia anayeitwa Quokka ameonekana kuwapiku wengine wote kwa kuchaguliwa kuwa ni mnyama mwenye furaha kuliko wote Duniani.
 
Mnyama huyu amekuwa akipendwa sana na watu mbalimbali hususani watalii katika upiga naye picha kutokana na uwezo mkubwa wa kuonyesha sura yenye furaha au tabasamu.
 
 
 
 
Quokka siyo mnyama mkali, nanirahisi sana kuanzisha naye urafiki. Kutokana na hili wanyama hawa wamepungua kwa kiasi kikubwa sana mara baada ya mbwa mwitu kuvamia misitu ya Australia.
Kwa sasa ni kati ya wanyama hadimu duniani na hatua mbalimbali zinachukuliwa ili kukinusuru kizazi chao.


 


 
 
 
 
 
 

 

 


No comments :

Post a Comment