Friday, July 10, 2015

Dawa inayopunguza makali ya saratani

Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la asili,uko katika awamu ya kwanza lakini homoni za Progesterone zinaweza kutumika kupunguza ukuwaji wa uvimbe.
Watafaiti hao kutoka nchini Uingereza na Australia wanasema kuwa matokeo hayo ni muhimu na sasa wanaanda majaribio yake.

Utafiti wa saratani nchini Uingereza unasema kuwa utafiti huo ni muhimu sana na unaweza kuwasaidia maelfu ya wanawake.
Homoni huchangia pakubwa katika saratani ya matiti.
Zinaweza kuigawanya seli ilio na saratani kupitia kukutana na seli inayoweza kutoa ishara katika sehemu ilioathirika na saratani.
Ufanisi mkuu wa dawa hiyo ya saratani,tamoxifen ni kukabili homoni ya oestrogen.Saratani yenye seli za homoni ya progesterone haina madhara makubwa.
Na sasa kundi moja la watafiti katika chuo kikuu cha Cambridge pamoja na kile cha Adelaide wametafiti kuhusu seli za saratani zinazokuwa katika maabara.
Zinaonyesha kuwa seli zenye homoni za progesterone pamoja na oestrogen zina uhusiano wa karibu na kwamba seli hizo za homoni ya progesterone zinaweza kupunguza madhara yanayosababishwa na seli za oestrogen.
Seli za saratani zinazokuwa katika maabaara zilikuwa nusu yake zilipotibiwa na progesterone na dawa ya tamoxifen ikilinganishwa na dawa ya tamoxifen pekee.
Mmoja wa watafiti ,profesa Carlos Caldas kutoka chuo kikuu cha Cambridge ameiambia BBC :inaonekana kwamba unaweza kudhibiti uvimbe huo vizuri,lakini ili kubaini iwapo inafanya kazi vyema miongoni mwa wanawake walio na saratani ya matiti ni lazima tuifanyie majaribio.
Watafiti hao wako katika awamu ya kwanza ya kuandaa majaribio.
Asilimia 75 ya wanawake wana saratani ya matiti ilio na seli zilizo na homoni za Oestrogen na vilevile asilimia hiyo pia ina seli zenye homini za Progesterone.

No comments :

Post a Comment