Friday, July 3, 2015

Upinzani ‘walianzisha’ tena bungeni


 
Dodoma. Mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika jana ulizua kizaazaa na kumlazimisha Spika Anne Makinda kuahirisha kikao baada ya kukosekana utulivu ndani ya Ukumbi wa Bunge.
Kikao hicho kiliahirishwa muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu wakati Bunge lilipotakiwa kukaa kama kamati kumalizia kiporo cha Muswada wa Sheria ya Kuwalinda Watoa Taarifa za Uhalifu na Mashahidi wa mwaka 2015 ambao mchakato wa kuupitisha haukukamilika juzi kutokana na muda kuisha.
Ilikuwa ni kama marudio ya hali ilivyokuwa mwishoni mwa mwaka jana wakati wabunge wa upinzani waliposimama na kuweka mazingira ambayo yalizuia shughuli za chombo hicho kuendelea wakati wa kujadili sakata la escrow.
Pages: 2 3

No comments :

Post a Comment