Friday, July 17, 2015

AJALI YA DALADALA NA FUSO YAUA WANNE NA KUJERUHI 11

WATU wanne wamefariki dunia na wengine 11 wakijeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea Wilaya ya Hai, Kilimanjaro ikihusisha gari aina ya Hiace iliyokuwa ikifanya safari zake kati ya Sanya Juu na Moshi baada ya kugongana na Fuso.

Kamishna Msaidizi wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Fulgence Ngonyani, amesema ajali hiyo imetokea saa moja asubuhi, ambapo majeruhi nane wamelazwa katika Hospitali ya Mawenzi na (KCMC) kwa matibabu na baadhi yao hali zao ni mbaya.


No comments :

Post a Comment