Saturday, July 18, 2015

ALIYEKUA MLINZI WA DR. SLAA KWA TAKRIBANI MIAKA 14 AHAMIA ACT-MAENDELEO


Wakati chama cha ACT- Maendeleo kikiendelea kujizolea wanachama, aliyewahi kuwa mlinzi wa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Khalid Kagenzi naye alionekana katika ofisi za ACT-Maendeleo.

Alipoulizwa na waandishi wa habari kama amehamia Kagenzi alijibu:

 “Ni haki ya kila Mtanzania kujiunga na chama chochote cha siasa anachokitaka. Bado sijachukua kadi yangu ya uanachama,”
Tujikumbushe kuhusu Kagenzi:

Kagenzi alikuwa ni mlinzi wa Dr. Slaa kwa takribani miaka 14, ambapo kibarua chake kiliingia matatani mara baada ya kutuhumiwa kutaka kumuua Dr. Slaa kwa sumu aliyopewa na viongozi wa CCM.

Kama unataka kujikumbusha zaidi, Bonyeza HAPA

No comments :

Post a Comment