Monday, July 20, 2015

JERRY SLAA APATA KIGINGI

Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa, amejikuta akiwa katika  wakati mgumu baada ya kumpata mpinzani wake Mwalimu wa Kitengo cha Kompyuta toka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Anthony Kalokola kwenye  kinyang’anyiro cha Ubunge katika
Jimbo la Ukonga. 

 
Jimbo hilo limekuwa wazi tangu Juni 2, mwaka huu  alipofariki  Mbunge wa Jimbo hilo, Eugen Mwaiposa, nyumbani kwake mjini Dodoma, hivyo wakazi wengi walimpatia nafasi Meya huyo kutokuwa na mpinzani.
 
Wakazi  wa jimbo hilo walikuwa kimya kwa kipindi fulani bila kujihusisha na shughuli za kisiasa, lakini  imewashangaza kipindi hiki  watu  kujitokeza  kutimiza  wajibu wao kikatiba   kwa  kugombea nafasi mbalimbali, ikiwamo ubunge na udiwani.
 
Kalokola ambaye ni mmoja  wa wagombea alisema yeye ameamua kuchukua na  kurejesha fomu ili  kugombea nafasi ya ubunge , hivyo hawezi kuzungumza chochote   bali Ilani ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM)  itawapatia nafasi ya kuzungumza chochote, lakini kiongozi  yeyote anapaswa kuwa mbunifu.

No comments :

Post a Comment