Monday, July 13, 2015

MEMBE , KIGWANGALA WANYOOSHA MIKONO

Waziri wa Mambo ya nje na  Ushirikiano wa  Kimataifa Mh. Bernard Membe  pamoja na  Mbunge wa Nzega  Dkt. Hamisi Kigwangalla wamekubali kushindwa katika kinyang’iro cha kuomba ridhaa ya kuteuliwa ndani ya chama cha Mapinduzi CCM zoezi lililohitimishwa leo.

Akizungumza na Mwandishi wetu mara baada ya Magufuli kutangazwa mshindi  , Mh. Bernad Membe amesema angechaguliwa mtu mwingine pasinge tosha leo katika ukumbi mpya wa chama cha Mapinduzi CCM, lakini kuteuliwa kwa Dkt Magufuri ameridhika kabisa kutoka ndani ya moyo wake huku akimmwagia  sifa Magufuli na kusisitiza kuwa  watanzania wamepata mtendaji shupavu.

Naye Kigwangalla amesema  hakika Magufuli ni chaguo la Mungu kwa  kuwa ni mmoja kati ya wanasiasa ambao hawajatoa hata shilingi kumi kuwapa wadhamini ili adhaminiwe kama ilivyo kwa wanasiasa wengine.

Kwa mujibu wa Nape Nnauye katibu wa Itikadi na Uenezi CCM  mara baada ya kumpata mwanasiasa atakaye peperusha bendera ya chama cha Mapinduzi amesema wanatarajia kufanya mkutano jijini Dar es salaam siku ya jumanne.

No comments :

Post a Comment