Monday, July 13, 2015

TAARIFA KAMILI KUHUSU TUKIO LA UJAMBAZI LILILOTOKEA USIKU WA JANA

WATU wanaodhaniwa kuwa majambazi wamevamia Kituo cha Polisi Stakishari kilichopo Ukonga jijini Dar es Salaam, jana usiku na kuua askari na raia kisha kupora silaha.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa watu hao walifika kituoni hapo wakiwa katika pikipiki wakidai kwamba walikuwa wamembeba mtu aliyepata ajali wakihitaji msaada wa polisi kabla ya kuwabadilikia ghafla na kuanza kuwashambulia kwa risasi.

Inadaiwa kuwa askari wanne wamepoteza maisha katika tukio hilo, wananchi wawili na mmoja wa magaidi hao.

Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema atakuwa na mkutano na wanahabari kati ya saa 5 au 6 leo kwa ajili ya kutoa taarifa rasmi juu ya tukio hilo la kigaidi.

No comments :

Post a Comment